STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, April 19, 2013

Golden Bush wazee kwa vijana kuonyeshana kazi kesho

Golden Bush Veterani

Golden Bush Fc

BAADA ya kutoka Morogoro wakiwa wameacha kumbukumbu ya kutoa kipigo uwanja wa Jamhuri, wakali wa soka la maveterani jijini Dar es Salaam, Golden Bush Veterani kesho asubuhi wanatarajiwa kuvaana na vijana wao wanaotisha kwenye Ligi Daraja la Nne Wilaya ya Kinondoni, Golden Bush Fc.
Pambano hilo la kirafiki la kujipima nguvu kuziweka vyema timu hizo katika michuano inayoshiriki, utachezwa majira ya saa 1 asubuhi kesho kwenye viwanja vya Chuo Kikuu (UDSM).
Msemaji wa timu hiyo, Onesmo Waziri 'Ticotico' alisema kuwa pambano hilo kwao ni maalum kwa ajili ya kujianda na mchezo wao dhidi ya mahasimu wao, Wahenga Fc watakaoumana nao siku ya Muungano.
Ticotico ambaye ni mmoja wa washambuliaji wa timu hiyo alisema kuwa wanaamini pambano lao litakuwa tamu ikizingatiwa vijana wao wanafanya vyema kwenye ligi hiyo ya TFF ikiongoza msimamo wa kundi lake ikiwa na pointi 12 kutokana na kushinda mechi zake zote nne ilizocheza mpaka sasa huku ikiwa na hazina kubwa ya mabao ya kufunga na kufungwa idadi ndogo ya mabao.
Timu hizi kwa hivi karibuni zilishakutana na mara ya kwanza wazee walichezea kichapo kabla ya kurudiana nao na kuwanyuka vijana hao mabao 2-1.
Ticotixo alisema wazee watakishusha kikosi chao chote kikali ili kuwatia adabu vijana wao ambao wameanza kuchonga kwa mafanikio yao ya kwenye ligi.

No comments:

Post a Comment