STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, April 19, 2013

Twanga Pepeta kusindikiza Utamaduni wa Msukuma Kirumba

 
BENDI ya muziki wa dansi ya African Stars 'Twanga Pepeta' ni miongoni mwa makundi yatakayotoa burudani katika tamasha kihistoria la 'Utamaduni wa Msukuma' litakalofanyika Mei 27 kwenye Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.
Mraribu wa tamasha hilo kutoka kampuni ya May Way Entertainment, Rose Mwita, alisema kuwa mbali na Twanga Pepeta ambayo itatumbuiza pia kwenye mwendelezo wa tamasha hilo mjini Nansio, Ukerewe siku ya Mei 28, pia kutakuwa na wasanii mbalimbali wa muziki wa kizazi kipya wakiwamo wanaotoka jijini Dar es Salaam.
“Tamasha hili linalenga kuhamasisha jamii ya Wasukuma, Wakerewe na makabila mengine kuenzi mila na tamaduni zetu. Vilevile, jamii na familia zilizopo ndani na nje ya mikoa  zikumbuke nyumbani na kutembelea wazee mara kwa mara,” alisema Rose.
Aliongeza kuwa wakati wa tamasha hilo, pia watakaohudhuria watapata nafasi ya kusikia historia ya Wasukuma na Wakerewe kwa kina kutoka kwa wazee wanaotoka maeneo mbalimbali, hasa kwenye familia za watemi wa Kisukuma na Kikerewe.
Maonesho mengine yatakayokuwapo wakati wa tamasha ni pamoja na maonyesho ya zana za kale za jadi zilizotumiwa na makabila hayo, kucheza ngoma za asili za Wasukuma na Wakerewe pamoja na vikundi tofauti vya ngoma za asili na sanaa za makabila mengine.
"Pia kutakuwa na vyakula vya aina mbalimbali vyenye asili ya Usukumani na Ukerewe... na pia vinywaji vya asili ya Msukuma na Mkerewe," alisema Rose.

No comments:

Post a Comment