STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, April 19, 2013

Van Persie, Suarez, Bale kuwania tuzo ya PFA

Robin Van Persie akiwa na tuzo ya PFA ya mwaka jana

KIUNGO nyota wa Tottenham Hotspurs, Gareth Bale, Luis Suarez wa Liverpool na Mholanzi Robin van Persie wa Manchester United wanatarajia kuonyesha kazi katika kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa Mwaka (PFA) iliyotangaza kwa msimu wa mwaka 2012-2013
Orodha iliyotangaza leo Ijumaa imetaja majina ya wachezaji sita wakiwemo hao watatu ambao wamekuwa moto msimu huu katika Ligi Kuu ya England.

Orodha hiyo imewajumuisha pia wakali wengine watatu ambao ni pamoja na Michael Carrick wa Manchester United, Eden Hazard na Juan Mata wa Chelsea.
Hata hivyo mshambuliaji wa Swansea City, Michu mwenye mabao 17 katika Ligi Kuu ya England yeye hayupo katika orodha hiyo kama ilivyo kwa nyota yeyote wa Manchester United..
Bale aliyeshinda tuzo hiyo mwaka 2011, ameteuliwa kutokana na mafanikio makubwa aliyoipa timu yake, ila anatarajiwa kupata upinzani toka kwa Suarez aliyeifungia Liverpool mabao 22 mpaka sasa katika Ligi Kuu.
Mshindi wa tuzo hiyo wa mwaka jana, Van Persie anayechuana na Suarez katika ufungaji wa mabao msimu huu akizidiwa kwa bao moja yeye na Carrick wanakaribia kuipa timu yao taji ya 20 la Ligi Kuu.

Hazard na Mata wapo katika orodha hiyo kutokana na kuisaidia timu yao katika msimu huu baada ya awali kuregarega.
Katika orodha wa Tuzo ya Mchezaji Bora Chipukizi ya Mwaka wapo Romelu Lukaku anayekipiga kwa mkopo West Brom na mshambuliaji wa Aston Villa, Christian Benteke.
Wachezaji wengine wanaokamilisha orodha hiyo ni wachezaji wa kimataifa wa England Danny Welbeck na  Jack Wilshere.
Washindi wa tuzo hizo watatangazwa Aprili 28 mwaka huu.
 

Orodha ya washindi waliopita 2011-12: Robin van Persie (Arsenal)
2010-11: Gareth Bale (Tottenham)
2009-10: Wayne Rooney (Man Utd)
2008-09: Ryan Giggs (Man Utd)
2007-08: C Ronaldo (Man Utd)

No comments:

Post a Comment