STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, May 28, 2013

Breaking Newssss:Albert Mangwea afariki Afrika Kusini, inadaiwa kalishwa sumu

Albert Mangwea enzi za uhai wake
NYOTA wa nyimbo za Ghetto Langu, Mikasi, Nipe Deal na nyinginezo, Albert Mangwea 'Ngwair' amefariki dunia leo saa 9 alasiri akiwa nchini Afrika Kusini kwa kile kilichoelezwa huenda alilishwa sumu.
Taarifa zilizotufikia hivi punde zinasema kuwa Ngwair tangu alipolala usiku wa jana hakuweza kuamka na wenzake waliokuwa wameambatana nchini humo waliamua kumgongea na walipoingia ndani walimkuta katulia na kumkimbiza hospitali moja mjini Pretoria na kugundulika kuwa amefariki baada ya kupimwa na daktari aliyempokea hospitalini hapo.
Japo taarifa zingine zinasema kuwa Ngwair na msanii mwenzake alioenda nchini humo kufanya Show M to the P walijidunga 'unga' na kusababisha mkali huyo wa hip hop kuaga dunia na mwenzake kuwa taaban.
Tayari inaelezwa msiba wa msanii huyo umewekwa mjini Morogoro baada ya taarifa hizo kufika kwa mama yake anayeishi huko.
Mungu aiweze roho yake mahali pema na MICHARAZO inafuatilia zaidi taarifa hizo kujua ukweli.

No comments:

Post a Comment