STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, May 28, 2013

Wakongo wanne wajitokeza kuomba kazi Msimbazi


Wachezaji wa Simba wakijifua

Tutamvutia tu Kibadeni! Ndivyo wachezaji wapya wanaoomba kazi Mismbazi wakijifua kabla ya kuangaliwa na kocha Kibadeni

Kibadeni akiwahakiki wachezaji wapya walijitokeza kujaribiwa

Andika majina yako kamili: Kibadeni akiwaandikisha majina wachezaji

Add caption

Wachezaji wapya wakijifua

Mtacheza hivi: Kocha msaidizi, Seleman Matola kizungumza na wachezaji wapya waliojitokeza kujaribiwa huku King KIbadeni (wa pili kulia) akisikiliza kwa makini


Wachezaji wa Simba U20 na wapya wakipimana ubavu leo uwanja wa Kinesi

Wachezaji wa Simba wakionyeshana kazi mazoezini leo asubuhi

Matola akitetea jambo na wanahabari

Mimi ndio Matola Bwana! Kocha wa U20 Seleman Matola akimueleza jambo Mahmoud Zubeiry mwenye miwani,  huku Saleh Ally akicheka kando yao

Wachezaji wapya wa Simba wakipashga moto uwanja wa Kinesi
WACHEZAJI wanne kutoka nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo (DR Congo), wakiwamo watatu wanaokipiga AS Vita wamejitokeza kuomba kibarua cha kuichezea Simba kwa msimu ujao ambao asubuhi ya leo walikuwa wakijaribiwa na kocha mpya wa timu hiyo, Abdallah Kibadeni 'King Mputa'.
Pia katika majaribio hayo wapo wachezaji wengine kadhaa akiwamo Mtanzania aliyekuwa akiichezea timu ya Ferreviario de Nampula ya Msumbuji, Miembeni Zanzibar na wachezaji wengine chipukizi kutoka jijini Dar katika klabu za Fc Boom ya Ilala, Buza Sports na Mbagala Scaret Academy.

Wachezaji kutoka Kongo wakiwamo washambuliaji watatu ni pamoja na Joe Fils kutoka Le Verez Club, Fabian Tshayaz, Fabrice Balou na Patrick Milambo wote wa AS Vita.
Wengine waliojitokeza kuomba 'kazi' Msimbazi ni Ramadhani Kipicha kutoka klabu ya Buza, Adeyun Saleh wa Miembeni Zanzibar, Mohammed Abdallah aliyekuwa anacheza Ferreviario De Nampula ya Msumbiji, Shaaban Kondo wa Mbagala Scalet Academy na Shaaban Said wa Fc Boom ya Ilala.
Wachezaji hao walisema wamejitokeza kuomba nafasi ya kufanya kazi Msimbazi kwa kuamini wanaweza licha ya kudai jukumu la kupima uwezo wao lipo mikononi mwa makocha wao, King Kibadeni, Jamhuri Kihwelu 'Julio', Seleman Matola na wote waliopo kwenye benchi la ufundi la timu hiyo.

Wakati wa maharibio hayo wachezaji wao walipewa muongozo na kocha wa timu ya vijana, Seleman Matola kabla ya Kibadeni kuzungumza nao huku wakishuhudiwa na Katibu Mkuu wa klabu hiyo, Evodius Mtawala aliyefika mapema uwanja wa Kinesi kwa ajili ya kuona kazi zinaendeleaje.

No comments:

Post a Comment