STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, May 28, 2013

Dekula Band kufanya makamuzi Little Nairobi




Dekula Kahanga 'Vumbi'

MKALI wa zamani wa bendi ya Orchestra Marquiz Original 'Wana Sendema', Alain Dekula Kahanga 'Vumbi' pamoja na kundi lake la Dekula Band wakiwa na wakali kama Lady Neema, Bobo Sukari na Yaya Sella wikiendi hii wataendelea na makamuzi yake nchini Sweden wanapoendelea na shughuli zao za muziki.
Vumbi aliiambia MICHARAZO kuwa Dekula Band 'Ngoma ya Kilo' watakamua burudani katika ukum,bi wa Lila Wien, maarufu kama Little Nairobi, wakiangusha ngoma mpya na za zamani mwanzo mwisho.
Maonyesho hayo yatafanyika kwa siku mbili mfululizo Mei 31 na Juni Mosi na kusema mashabiki wa bendi hiyo na waliozoea ukumbi huo hawapaswi kuikosa burudani hiyo itakayoambatana na show kabambe pamoja na kukumbushiwa vibao vya zamani vilivyomfanya yeye wenzake kuwatamba nchini enzi zao.
Vumbi alisema wamepania kufanya mambo makubwa zaidi ya yaliyozoeleka kufanywa na bendi yake.

Tangazo lao linasomeka hivi;
"Wazee Wapewe" present's;
Lady Neema,Bobo Sukari & Yaya Sella
Dekula Band"Ngoma Ya Kilo"
Place: Lilla Wien"Little Nairobi"
Date: 31/may & 01/june/2013
Time: 21.00-01.00
Addr: Swedenborgsg.20
Pendel: Södra station
http://www.youtube.com/watch?v=T3KIYgRlyR0

No comments:

Post a Comment