STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, May 31, 2013

Mwili wa Ngwair sasa kuwasili J'pili, mazishi yake J'4

Ngwair enzi za uhai wake


MWILI wa marehemu Albert Mangwea 'Ngwair', aliyekuwa nyota wa muziki wa kizazi kipya kupitia miondoko ya Hip Hop, hautawasili tena kesho kama ilivyokuwa imepangwa na badala yake utawasilia siku ya Jumapili na kuagwa Jumatatu kabla ya kusafirishwa kwenda kuzikwa siku ya Jumanne mjini Morogoro.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa hivi punde na Kamati ya Mazishi ya msanii huyo aliyefariki nchini Afrika Kusini, imesema sababu ya mwili wa Ngwair kurejeshwa kesho umetokana na watanzania waliopo nchini humo kuomba wapewe nafasi ya kumuaga kesho ndipo usafirishwe kuja Tanzania.
Taarifa inasema kuwa watanzania hao ambao kwa namna moja au nyingine wamekuwa mstari wa mbele katika kuratibu shughuli zote tangu Ngwair apelekwe hospitali mpaka kufariki kwake na kuhamishwa hospitali aliyokuwa amehifadhiwa na kupelekwa hospitali ya Serikali hivyo wameona ni vyema nao wakamuaga mpendwa wao.
Kutokana na ratiba hiyo kupanguliwa utaratibu kwa sasa ni kwamba Jumamosi mwili huo wa Ngwair utaagwa Afrika Kusini na kusafirishwa kurejeshwa Tanzania ambapo utawasilia Jumapili saa 8 mchana kabla ya kupelekwa moja kwa moja Muhimbili kuhifadhiwa.
Jumatatu kuanzia saa 2 mpaka saa 6 mashabiki wa muziki watauaga mwili huo kabla ya kuanza safari ya kupelekwa Morogoro kwa mazishi.
Kamati hiyo imesisitiza watanzania waendelea kujitolea michango kwa ajili ya kufanikisha mazishi ya Ngwair kwa kutuma fedha kwa simu ya kaka wa marehemu Kenneth Mangwea 0754-967738 au katika akaunti ya namba 2012505840 Benki ya NMB kwa jina la Kenneth B Mwangweha.
Katika hatua nyingine, msanii aliyekuwa hoi pamoja na Ngwair, M2P anaendelea vyema ambapo hivi punde amehojiwa 'live' na Clouds FM na kusema anaendelea vizuri japo anasumbuliwa na maumivu ya kichwa na kifua na ameanza kunywa vitu vyepesi  na anamshukuru Mungu hali yake inatengemaa.
Hata hivyo ni kwamba M2P hajui chochote kinachoendelea juu ya kifo cha Ngwair kwa vile walimuongopea kwamba rafikie amerejea Tanzania wakati yeye akiwa katika hali mbaya ya kiafya.

No comments:

Post a Comment