STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, May 31, 2013

Neymar: Nahisi kutetemeka kucheza na Messi

http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/3/3e/Messi_with_Neymar_Junior_the_Future_of_Brazil.jpg
Messi na Neymar
RIO DE JANEIRO, Brazil
MSHAMBULIAJI mpya wa Barcelona, Neymar amesema anajihisi "kupagawa" kila anapofikiria kuja kucheza pamoja na Lionel Messi.
Mbrazil huyo mwenye umri wa miaka 21, ambaye alibainisha wiki iliyopita kwamba anajiunga na mabingwa wa La Liga kwa dili la uhamisho la paundi milioni 28, alisema kuwa wakati umefika wa kuja kuwa nyota wa soka la Ulaya.
Akizungumza katika uzinduzi wa viatu vya Nike Hypervenom, Neymar alisema: "Najisikia kupagawa. Hii ni ndoto iliyokuwa kweli. Kucheza na Messi na wachezaji wengine wenye vipaji pale Barcelona ni jambo lililonifanya nichague kujiunga nao."
Nyota huyo pambo la soka la Brazil alipata ofa kutoka katika klabu kadhaa zikiwamo Real Madrid na Chelsea lakini alichagua kwenda kucheza na 'fundi' wa Kiargentina Messi klabuni Nou Camp baada ya kujadiliana na familia yake.
"Yalikuwa maamuzi magumu lakini niliamua pamoja na familia yangu,” alibainisha. “Walinisaidia sana. Nina furaha lakini pia huzuni kwa kuondoka katika timu (Santos) ambayo nimekuwa kwa miaka mingi. Natakiwa kuitumia fursa."
Neymar aliongeza kwamba baada ya uhamisho wake sasa anaweka akili zake katika kuitumikia timu ya taifa ya Brazil, huku michuano ya Kombe la Shirikisho ikitarajiwa kuanza Juni 15.
"Kuvaa jezi ya njano ni majukumu lakini unatakiwa kuivaa na kucheza kama vile unacheza uani kwako,” alisema. “Unatakiwa uwe na furaha.
“Daima nimekuwa nikitaka kuchezea Brazil na kuwa mchezaji kama Ronaldo, Ronaldinho na pia Robinho na Kaka - kuna wachezaji wengi sana ninaopwapenda."

RONALDINHO
Mwanasoka bora wa zamani wa dunia, Ronaldinho (33) amepongeza uhamisho wa Neymar kutua katika klabu yake ya zamani ya Barcelona.
Ronaldinho anaamini kwamba Neymar atafurahia soka la Ulaya kwa sababu ana kipaji kinachohitajika kuwa mmoja wa wachezaji bora duniani.
Macho yote yameelekezwa kwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 21 baada ya kukamilisha uhamisho wake wa kwenda Barcelona, na Ronaldinho, ambaye aliichezea barca kwa miaka mitano, anaamini kwamba yosso huyo atatamba Ulaya
"Itakuwa jambo zuri kumuona akiichezea Barcelona," Ronaldinho aliwaambia waandishi wa habari wa Brazil. "Barca ni klabu kubwa katika moja ya ligi bora duniani.
"Atazoea kwa sababu ana kila kitu kinachohitajika kumfanya awe bora duniani."
Neymar anatarajiwa kutambulishwa Barcelona mapema mwezi ujao kabla ya kurejea kuatika maandalizi ya kuiwakilisha Brazil katika michuano ya Kombe la Shirikisho Juni 15.
Ronaldinho ameachwa nje ya kikosi cha kocha Luiz Felipe Scolari kitakachoshiriki michuano hiyo.

NEYMAR HABARI NYINGINE
Kocha wa timu ya taifa ya Hispania, Vicente Del Bosque amemsifu Neymar akisema ni "habari nyingine" na akiongeza kuwa "ni fundi mwenye uwezo mkubwa. Atafanya makuibwa."
Del Bosque pia anaamini kwamba yosso huyo Mbrazil hatapata shida kucheza pamoja na 'supastaa' wa Barca, Lionel Messi. "Tulikuwa na majina makubwa mengi katika chumba cha kuvalia wakati naifundisha Real Madrid na tulifanikiwa sana."

UTATA WA JEZI
Miamba hao wa Catalunya watalazimika kutafuta namba ambayo Mbrazil huyo anaipenda, jambo ambalo litakuwa gumu kwa sababu namba zinazomvutia ni 7 inayovaliwa na David Villa, 11 inayovaliwa na Thiago Alcantara.
Duka la klabu hiyo limeshaanza kuuza jezi zenye jina la Neymar lakini zikiwa na namba zote hizo mbili.

No comments:

Post a Comment