STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, May 31, 2013

Mzee Yusuf kupamba Miss Arusha Juni 8

http://www.gushit.com/files/bookmark_photos/7a6b3e0e06L.jpg
Mzee Yusuf
KUNDI la muziki wa taarabu linaloongozwa na muimbaji nyota wa miondoko hiyo nchini, Mzee Yusuf, Jahazi Modern inatarajia kuinogesha usiku wa kumsaka mlimbwende wa mkoa wa Arusha (Redds Miss Arusha) inatarajiwa kufanyika June 8 katika ukumbi wa triple A uliopo jijini humo.
Akizungumza na waandishi wa habari muandaaji wa shindano hilo Phidesia Mwakatalima alisema kuwa shindano hilo litafanyika usiku wa jumamosi june nane katika uwanja wa ukumbi wa Triple A uliopo ndani ya jiji la Arusha.
Alisema kuwa jumla ya walibwende kumi na tano 15 kutoka katika vitongoji vitatu vya jiji la Arusha ambapo alivitaja kuwa ni pamoja na kitongoji cha Njiro,Arusha mjini(Arusha city cetre)pamoja na kitongoji cha Monduli.
Alibainisha kuwa mpaka sasa warembo wameshaingia kambini wameanza kujifua kwa ajili ya shindano hilo huku akibainisha kuwa kwa mwaka huu lazima mrembo wa Tanzania (Redds Miss Tanzania )atokee mkoa wa Arusha.
Alisema kuwa zawadi mbalimbali zitatolewa ikiwemo kuwasomesha warembo katika vyuo mbalimbali lungha ya kiswahili, kingereza pamoja na kifaransa.
Kwa upande wa wadhamini waliothamini shindano hili walisema kuwa ni pamoja na perfect choice super markety, libeneke la kaskazini blog, triple A FM, Radio 5 FM, Sunrise FM, Mambo Jambo FM, Alayance france,Geo Securty,Cassaranda wear,Meru Spring Water Pamoja na Otakef
Motel.

No comments:

Post a Comment