STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, June 13, 2013

Fabregas azikata maini Man Utd, Arsenal

Cesc Fabregas

KIUNGO Cesc Fabregas amevunja ukimya na kusema kwamba hana mpango wa kuondoka Nou Camp, licha ya tetesi za kuwaniwa na mabingwa wa England, Manchester Utd na klabu yake ya zamani Arsenal.
Fabrega, 26, amesema licha ya tetesi hizo mipango yake ni kusalia Barcelona kipindi hiki cha majira ya Joto.
Alisema "Siku zote nimekuwa zikisema najisikia furaha kuwepo Barca. Wanaosema naondoka hawanijui na wala hawajazungumza nami,"
Akaongeza hakuna aliyezumnguza na wakala wale kwa sababu anajua namna gani sipendi azungumze na watu wengine kuhusu mimi.
Nyota huyo wa Hispania alisema huwa hapendi mambo yake binafsi kuwaambia wengine na hata hilo analopakaziwa sasa la kutaka kurejea Ligi Kuu ya England hajaiambia hata familia yake.
"Iwapo mtu mmoja amesema lolo kuhusu hilo amekosea, nataka kuendelea kucheza Barca, hivi ndivyo ilivyo," alisema Fabregas alikyehama Arsenal kutoa Barcelona Agosti 2011 kwa kitita cha Paundi Mil 30.

No comments:

Post a Comment