STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, June 13, 2013

Mhe Sugu, Sir Nature kumpiga tafu Anaconda Nyumbani Lounge

Jide katika pozi
MMOJA wa waasisi wa muziki wa kizazi kipya nchini ambaye kwa sasa ni Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini-ChADEMA, Mhe. Joseph Mbilinyi, Sir Juma Nature na Komandoo Hamza Kalala ni baadhi ya watakaomsindikiza onyesho la Lady Jaydee 'Anaconda' katika maadhimisho ya miaka 13 tangu ajitose kwenye fani hiyo.
Onyesho hilo la Anaconda maarufu kama Binti Machozi a.k.a Comandoo litafanyika kwenye ukumbi wa Nyumbani Lounge kuanzia saa 3 usiku ambapo mwanadada huyo ameanika hadharani mipango mizima ya onyesho lake hilo.
Kwa mujibu Jide kupitia akaunti yake ya Twitter ni kwamba kesho atapigwa tafu na Mh Sugu, mmoja wa watu waliomuibua kisanii.
Jide ambae hivi karibuni ameachia wimbo mpya unaopatikana kwenye album yake ‘Nothing but the truth’ inayoitwa Yahaya, amepost kupitia kupitia ukurasa wake wa facebook na pia katika akaunti yake ya Twitter kuonesha list ya wasanii watakaopanda jukwaani, na pia uwepo wa Sugu.
” Miaka 13 ya Lady JayDee, Ijumaa ya kesho shughuli inaanza rasmi saa 3:00 usiku...Ukiskia paaaa ujue show imeisha

1. Prof Jay 2. Juma Nature 3. Grace Matata 4. Hamza Kalala 5. Wakazi na ugeni wa Mh. Joseph Mbilinyi a.k.a SUGU

Nyimbo zote unazozipenda zitalia tar 14 June, pale Nyumbani Lounge sababu yaaaaa sababu yaaaaaa ?????????”
Sidhani kama utaikosa hafla hiyo ambayo itatumika pia kusimikwa rasmi kwa Jide jina la 'Komandoo' na mkongwe Hamza Kalala.

No comments:

Post a Comment