STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, June 12, 2013

Kijana mbaroni kwa kumchinja mfanyakazi mwenzake


Mwili wa Perpetua ulipotolewa katika shimo la taka na Polisi (Picha:Hisia za Mwananchi)

http://1.bp.blogspot.com/-MVUICKkwko4/UIFMQ3WHVbI/AAAAAAAB1uU/oRJvBq38NN8/s640/Kovakamanda.jpg
Kamanda Kova
JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam linawashikilia watu wanane, akiwamo mfanyakazi wa ndani anayetuhumiwa kumuua mfanyakazi mwenzake waliyekuwa wakifanya kazi nyumbani kwa Jaji Kileo kwa kumchinja kama kuku.

Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleiman Kova, alisema hayo alipozungumza na waandishi wa habari jana.

Alisema Philemon Laiza (27), mkazi wa Mikocheni B, anatuhumiwa kuhusika na mauaji ya Perptua Maina (30) kwa kumchinja na kisha kutelekeza mwili wake kwenye dampo la takataka.

Kova alisema mtuhumiwa anashikiliwa na Polisi na upelelezi utakapokamilika atafikishwa mahakamani.

Katika tukio la pili, alisema watu wawili; Isaya Mafuru (31) na Yusufu Machela (33), wanatuhumiwa kwa uporaji wa mali za raia wa Sweden, Gisela Bergstorm katika maeneo ya Coco Beach.

Katika tukio la lingine, alisema watu wanne, ambao ni Thenase Benjijimana (26), raia wa Burundi, Said Hassan (37), mkazi wa Mbande, Obadia Bukuku (25) na Benedict Mohamed (32) wakazi wa Tabata, wanatuhumiwa kwa kukutwa na gari ya wizi aina ya Noah T 157 BWC, pamoja na pikipiki aina ya Boxer T 568 CDL.

Wote kwa pamoja wanashikiliwa na Jeshi la Polisi kwa ajili ya upelelezi zaidi.

No comments:

Post a Comment