STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, June 12, 2013

Mwamuzi jela miezi 6 kwa kupanga matokeo ili apewe uroda


http://www.dutchreferee.com/wp-content/uploads/2013/03/ali-sabbagh-twitter-referee.jpg
Ali Sabbagh

REFA wa kimataifa na maarufu nchini Lebanon, Ali Sabbagh amehukumiwa kwenda jela baada ya kukutwa na hatia ya kupanga matokeo ya michezo uwanjani kwa malipo na ngono.
Kwa mujibu wa taarifa zilizoripotiwa na vyombo vya habari za nchini Singapore, mwamuzi huyo ambaye amekuwa akicheza mechi mbalimbali za kimataifa zikiwamo za kuwania kufuzu Fainali za Kombe la Dunia amekutwa na hatia hiyo yeye na wasaidizi wake wawili na mahakama moja nchini Singapore.
Sabbagh, 34 inadaiwa amekuwa akipanga matokeo kwa minajili ya kulipwa ujira wa ngono na wanawake aliokubaliana nao, jambo lililomshangaza jaji aliyekuwa akiisikiliza kesi hiyo na kutoa hukumu hiyo Jumatatu wiki hii akihojikama kesi hiyo tu katutwa na hatua je ni michezo mingapi amekuwa akilipwa ujira huyo wa kubadilisha mechi kwa ngono?
Wasaidizi wake waliohukumiwa miezi mitatu kila moja kwa makosa hayo ni  Ali Eid, 33, na Abdallah Taleb, 37.
Inaelezwa waamuzi hao walikutwa na hatia ya kupanga matokeo katika pambano la Kombe la Shirikisho kwa nchi za Asia lililofanyika Aprili 3, kati ya klabu ya Singapore Tampines dhidi ya East Bengal ya India, iliyoshinda mabao 4-2 dhidi ya wenyeji wao.
Waamuzi hao wanadaiwa walifanya mipango hiyo wakishirikiana na mfanyabiashara anayesifika kwa dili za upangaji matokeo nchini Singapore, Ding Di Yang kwa kukubaliana na wanawake kupanga matokeo ya pambano kwa kulipwa mapenzi.
Wakili wa mwamuzi huyo, Gary Low, alisema haoni sababu ya mteja wake kuadhibiwa iwapo hakunufaika kifedha na mchongo huo anaoshutumiwa kuufanya ambao ni tuki jipya katika rushwa michezoni.

No comments:

Post a Comment