STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, July 7, 2013

Azam Academy yaanza kwa kishindo michuano ya Rolling Stone

Azam Academy ilipokuwa ikijaindaa na michuano hiyo ya Rolling Stone
TIMU ya soka ya vijana ya Azam, Azam Academy, imeanza kwa kishindo michuano ya kimataifa ya vijana Afrika Mashariki na Kati, Rolling Stone baada ya kuikwanyua Eagle Rangers ya Tanga kwa mabao 3-0.
Azam ilijipatia mabao yake kupitia kwa wakali wake, Mange Chagula, Kevin Friday na Erick Haule na kuwaacha hoi vijana wenzao ambao wa Eagles iliyowahi kuchezewa na nyota kadhaa akiwamo Mchezaji Bora wa michuano ya Kombe la Taifa 2009, Salum Aziz Gillah aliyewahi kung'ara na Simba na Coastal Union.

No comments:

Post a Comment