STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, July 7, 2013

Nani wa Man United kutimkia As Roma

Nani
MSHAMBULIAJI wa pembeni wa Mabingwa wa Ligi Kuu ya England, Manchester United, Louis Nani anatarajiwa kujiunga na klabu ya AS Roma, wakala wa winga huyo kutoka Ureno, Jorge Mendes amefichua.
Wakala huyo alisema Nani mwenye miaka 26 yu njiani kuondoka Old Trafford na kujiunga na timu hio ya Italia, licha ya kwamba pia anahusisha na kunyemelewa na klabu za Galatarasay, Juventus, Arsenal na Real Madrid.
"Nani ni mchezaji mzuri na dunia yote inafahamu hili" alisema Mendes kabla ya kuongeza kuwa "Atajiunga na As Roma, kwa isiwe wakati Serai A ni bonge la Ligi bora duniani na jiji la Roma linavutia na kupendeza!" alisema Mendes.
Alisema alikuwa katika mipango ya kuonana na klabu ya United kwa lengo la kuweka mambo sawa ili Nani atimke zake katika klabu hiyo aliyobakisha mkataba wa mwaka mmoja tangu alipotua OT kwa kitita cha pauni Milioni 25.5 mwaka 2007.
Winga huyo amekuwa hana uhakika wa namba katika timu hiyo kwa misimu miwili iliyopita na kwamba aliwahi kuwekwa sokoni na kuelekea kutua Galatasaray kabla ya klabu hiyo ya Uturuki kushindwa kulipa kitita cha Pauni Milioni 8.5 kilichokuwa kikiitaka United.

No comments:

Post a Comment