STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, July 7, 2013

Kaseba aachia Bongo Mafia

BINGWA wa zamani wa dunia wa Kick Boxing Japhet Kaseba 'Champion' ameingia katika ulingo wa fani ya filamu baada ya kuachia mtaani filamu ya 'action' iitwayo 'Bongo Mafia' aliyoigiza na wasanii kadhaa wakongwe wa fani hiyo.

Filamu hiyo iliyorekodiwa na kukamilika hivi karibuni ipo mtaani kwa sasa baada ya kuachiwa wiki iliyopita ili mashabiki wa fani hiyo wapate burudani ambayo wamekuwa wakiikosa katika filamu za mapigano.
Picha hiyo ni mfululizo za filamu nyingine zilizopo njiani ambapo aliidokeza MICHARAZO kuwa 'Daddy Sin' kazi yake nyingine ipo katika maandalizi ya kutoka baada ya 'Bongo Mafia'.
Katika filamu hiyo ya sasa Kaseba kaigiza na wakali kama Dotnata Poshi, Ahmed Khalfan 'Kelvin', Abdallah Mkumbira 'Muhogo Mchungu', Pendo Njau, Rongers 'Master Shivo'  na wakali wengine.

No comments:

Post a Comment