STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, July 7, 2013

Wawili wafa, 182 wanusurika ajali ya ndege ya Asiana Airlines







WATU wawili wamefariki na wengine zaidi ya 180 kunusurika kufa katika ajali iliyohusisha ndege aina ya Boeing 777 ya kampuni ya Asiana Airlines, iliyoanguka ardhini katika kiwanja cha Kimataifa ccha Ndege cha San Francisco, Marekani.
Kwa mujibu wa CNN, ndege hiyo ilianguka na kulipuka moto ndani kwa ndani na kusababisha vifo vya watu wawili na wengine 182 kujeruhiwa na kukimbizwa hospitalini kwa matibabu zaidi.
Taarifa zaidi zinasema miongoni mwa abiria waliokuwa katika ndege hiyo ni wanafunzi wa sekondari 26 kutoka China ambao walikuwa wameenda katika mji huo kwa ajili ya kambi ya mapumziko kipindi hiki cha majira ya joto.

No comments:

Post a Comment