STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, July 6, 2013

Wanafunzi 29 na mwalimu wao wauwawa katika shambulio la kigaidi

Potiskum, Nigeria (AP)
WANAFUNZI 29 pamoja na mwalimu wao wameuwawa alfajiri ya leo Kaskazini mwa Naigeria kwa kile kilichoelezwa shambulio la kigaidi lililofanya na kundi la waasi la Boko Haram
Baadhi ya waathirika ambao bado wanatibiwa majeraha ya risasi na kuchomwa moto wamesema baadhi ya wanafunzi walichomwa moto wakiwa hai katika shambulio hilo kabla ya alfajiri ya Jumamosi (leo) katika shule ya sekondari ya serikali iliyopo mjini Mamudo jimboni Yobe.
Huku akitokwa na machozi ya uchungu pembeni ya miili ya wavulana wake wawili, mkulima Malam Abdullahi aliapa kuwaondoa wanae watatu waliobaki katika shule ya jirani.
Alilalamika kwamba kulikuwa hakuna ulinzi kwa ajili ya wanafunzi licha ya kupelekwa kwa maelfu ya askari tangu serikali ilipotangaza hali ya dharura katikati ya Mei katika majimbo matatu ya Kaskazini-mashariki.
Shule nyingi zimechomwa moto na idadi kubwa ya wanafunzi kuuawa wakiwamo zaidi ya waathirika 1,600 waliouawa katika matukio hayo ya kigaidi tangu 2010.

No comments:

Post a Comment