STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, July 6, 2013

RAIS KIKWETE KUCHEZESHA MECHI YA WABUNGE‏ SIMBA, YANGA

Rais Dk. Jakaya Mrisho Kikwete.
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Jakaya Mrisho Kikwete, amekubali kuwa mgeni rasmi katika Tamasha la Usiku wa Matumaini litakalofanyika kesho Jumapili katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam. Aidha, Rais atahutubia katika tamasha na pia atakuwa refa wa mechi za wabunge wa Yanga na Simba.
Mbali na pambano hilo tamasha hilo lenye lengo la kuchangisha fedha kwa ajili ya ujenzi wa mabweni ya wanafunzi wa kike wa Sekondari, kutakuwa pia na mipambano ya ngumi baina ya Wabunge na wasanii wa Bongo Movie.
Pia litakuwepo pambano la soka baina ya timu ya wasanii wa muziki wa kizazi kipya 'Bongofleva' na Bongo Movie sambamba na burudani nyingine ya muziki toka kwa wasanii mbalimbali wakiwemo wa muziki wa Injili na dansi. 

No comments:

Post a Comment