STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, July 6, 2013

Fainali za Airtel Rising Stars kurushwa live Supersport

Baadhi ya timu shiriki za michuano hiyo zikichuana uwanjani
FAINALI za michuano ya Airtel Rising Stars kwa wavulana na wasichana zinazofanyika leo kwenye Uwanja wa Karume jijini Dar es Salaam, zitaonyeshwa na kituo cha televisheni cha Supersport kuanzia saa 7:30 mchana.
Akizungumza jijini jana, Afisa Habari wa Shirikisho la soka (TFF), Boniface Wambura, alisema nusu fainali za mashindano hayo zilizofanyika jana zilihusisha timu za wasichana za Kinondoni iliyocheza na Kigoma wakati Temeke ilicheza na Ilala wakati kwa upande wa wavulana Mwanza ilicheza na Ilala huku Kinondoni ikiumana na Morogoro.
"Fainali kwa upande wa wasichana itaanza saa saba mchana na fainali ya wavulana yenyewe itaanza saa tisa na nusu alasiri hivyo wadau wa soka na mashabiki wajitokeze kwa wingi kuangalia fainali hizi," alisema Wambura.
Alisema kuwa maandalizi kwa ajili ya fainali hizo za leo yamekamilika ambapo wanategemea kuona vipaji vipya vya vijana.
Mashindano hayo ya soka ya vijana yanayofanyika kila mwaka yamedhaminiwa na kampuni ya huduma za simu ya Airtel.

No comments:

Post a Comment