STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, July 6, 2013

TFF yataja wakaoshiriki kozi ya ukocha ya FIFA

MAKOCHA wa mpira wa miguu na walimu 28 kutoka Shirikisho la Mpira wa Miguu (TFF) na shule za msingi na sekondari, wameteuliwa kuhudhuria kozi ya FIFA inayoanza kesho Hombolo mkoani Dodoma.
Taarifa ya TFF iliyotolewa jana ilisema kozi hiyo itakayomalizika Julai 20 itakuwa chini ya ukufunzi wa Rogasian Kaijage ambaye pia ni kocha wa timu ya taifa ya wanawake (Twiga Stars).
Kozi hiyo itatoa nafasi kwa walimu hao kuongeza ujuzi kwenye soka, taarifa ilisena na kuwataja washiriki wa kozi hiyo kuwa ni:
Abdul Mikoroti (Shule ya Msingi Nzasa), Baltazar Kagimbo (Shule ya Msingi Tabata Jica), Baraka Baltazar (Shule ya Msingi Muhimbili), David Kivinge (Shule ya Msingi Temeke) na Dismas Haonga (Tambaza Sekondari).
Wengine ni Exuperus Kisaka (Shule ya Msingi Mavurunza) na Hadija Kambi (Shule ya Msingi Karume).
Wengine ni pamoja na Hamis Chimgege (Shule ya Msingi Tusiime) na Hobokela Kajigili (Shule ya Msingi Buguruni).
Wengine zaidi ni Issack Mhanza (Shule ya Msingi Airwing), Job Ndugusa (Shule ya Msingi Upanga), John Sebabili (TFF), Lutta Rucharaba (Shule ya Msingi Montfort) na Maua Rahidi (Shule ya Msingi Uhuru Wasichana).
Taarifa ya TFF iliwataja washiriki zaidi wa kozi hiyo kuwa ni Michael Bundala (TFF), Mussa Kapama (Shule ya Msingi Bunju ‘A’), Priscus Silayo (Shule ya Msingi J.K. Nyerere), Peter Manyika (TFF) na Rajabu Asserd (Shule ya Msingi Mtoni Kijichi).
Wengine ni Raphael Matola (TFF), Raymond Rupia (St. Anne Maria Academy), Renatus Magolanga (Ulongoni Sekondari), Ruth Mahenge (Shule ya Msingi Chang’ombe), Said Pambaleo (TFF), Sebastian Nkoma (TFF), Titus Michael (TFF) na Wane Mkisi (Jangwani Sekondari).

No comments:

Post a Comment