STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, July 6, 2013

Sylona ndiye Redd’s Miss Temeke 2013

Mshindi wa Redds Miss Temeke 2013, Sviona Nyameyo (katikati), akiwa na mshindi wa pili,  Narietha  Boniface na mshindi wa tatu,  Latifa Mohamed mara baada ya kutangazwa washindi katika shindano hilo lililofanyika jana TCC Chang'ombe.

KISURA Sylona Nyameyo jana usiku alifanikiwa kutwaa taji la Redd’s Miss Temeke lililofanyika katika Ukumbi wa TCC Changombe, jijini Dar es Salaam.
Sylona mwanafunzi wa mwaka wa kwanza katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), akisomea mambo ya sheria alifanikiwa kuwashinda warembo wengine na kufanikiwa kujitwalia taji hilo.
Katika shindano hilo lililokuwa na upinzani mkali, ulioambatana na burudani za kumwaga, ilishuhudiwa nafasi ya pili ikienda kwa Marietha Boniface, ambaye naye ni mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Sayansi na Tiba Muhimbili (MUCHS).
Nafasi ya tatu ilikwenda kwa Latifa Mohammed ambaye amemaliza kidato cha sita mwaka huu, hivyo warembo hao kujihakikishia nafasi ya kuingia katika fainali za Redd’s Miss Tanzania.
Ushindani ulionekana dhahiri katika shindano hilo, ambapo warembo walikuwa wakichuana mno, huku mashabiki waliojitokeza hapo wakijikuta wakishangilia muda wote.
Akizungumza mara baada ya kuvikwa taji hilo, Sylona alisema amefurahishwa mno na matokeo hayo na atahakikisha hawaangushi wakazi wa Temeke katika shindano la Redd’s Miss Tanzania.
“Nilijua toka mwanzo lazima niwashinde, maana nilijiamini na niliona nina vigezo vyote, sasa ni wakati wa kwenda kupambana katika Redd’s Miss Tanzania ili kurudisha heshima ya Temeke,” alisema.
Shindano la Redd’s Miss Tanzania kwa sasa linadhaminiwa na kinywaji cha Redd’s Original kinachozalishwa na kusambazwa na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL).

No comments:

Post a Comment