STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, July 6, 2013

Warundi kuichezesha Stars na Waganda Jumamosi ijayo


Kikosi cha Stars
SHIRIKISHO la soka barani Afrika (CAF) limeteua waamuzi kutoka Burundi kuchezesha mchezo wa kwanza wa mchujo kwa ajili ya fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika kwa wachezaji wa ligi za nyumbani (CHAN) kati ya Taifa Stars na Uganda.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini jana, Afisa Habari wa Shirikisho la soka (TFF), Boniface Wambura, aliwataja waamuzi hao kuwa ni mwamuzi wa kati Thierry Nkurunziza na wasaidizi wake Jean Claude Birumushahu na Pascal Ndimunzigo.
Wambura alisema mwamuzi wa akiba ni Pacifique Ndabihawenimana wakati kamishna ameteuliwa kuwa Gebreyesus Tesfaye kutoka Eritrea.
Tesfaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Miguu cha Eritrea na mjumbe wa Kamati ya Maandalizi ya Mashindano ya CHAN.
Kikosi cha Taifa Stars ambacho kipo kambini kwa sasa kitaumana na Uganda Jumamosi kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam kabla ya kurudiana ugenini wiki mbili baadae.
Endapo Stars itafanikiwa kupata matokeo mazuri kwenye michezo hiyo miwili dhidi ya Uganda itakuwa imefuzu kushiriki kwa mara ya pili kwenye mashindano hayo.
Wakati huo huo, CAF pia imemteua Mtanzania Leslie Liunda kuwa Kamishna wa mechi kati ya Burundi na Sudan itakayochezwa jijini Bujumbura, Afisa Habari wa Shirikisho la soka (TFF), Boniface Wambura alisema.
Mechi hiyo ya kwanza ya mchujo ya CHAN itafanyika kesho Julai 7.

No comments:

Post a Comment