STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, August 21, 2013

Arsenal Wenger asalimu amri, atangaza kuingia sokoni kusaka nyota

http://images.football365.com/12/11/800x600/Manchester-United-v-Arsenal-Arsene-Wenger-pa2_2855230.jpg 
LONDON, England
BAADA ya kuona mambo yanamwendea vibaya na hana njia nyingine ya kunusuru ajira yake Arsena, Kocha Arsene Wenger ametangaza kurejea sokoni kusaka wachezaji akitumia akiba aliyonayo ya Pauni Milioni 65.

Wenger ambaye kipigo cha mabao 3-1 toka kwa Aston Villa kimemweka pabaya mbele ya mashabiki wa klabu hiyo ya Emirates alitangaza uamuzi huo usiku wa kuamkia juzi.
 
Kocha huyo alisema kuwa bado anatafuta ufumbuzi mwingine na kwamba atazitumia fedha hizo kwa ajili ya kusaka nyota wengine kwenye michuano hiyo ya Ligi Kuu ya England.
 
Kwa sasa Gunners imeshatangaza dau la pauni milioni 12 ikimsaka kiungo wa timu ya Taifa ya Ufaransa, Yohan Cabaye dau ambalo limekataliwa na  Newcastle ambayo inataka dau hilo liongezeke zaidi.

Hata hivyo kwa mujibu wa  Starsport klabu hiyo iliyokumbwa na mgogoro inawawinda nyota wengine watatu ambao huenda wakaigharimu pauni hizo milioni 65.

Wanaotajwa kuwa mawindo ya timu hiyo ni nyota wawili wa timu ya  Swansea, Michu na  Ashley Williams pamoja na nyota wa Manchester City, Micah Richards, ambaye mwenyewe binafsi anataka kujiunga na  Gunners.

Awali kabla ya kutangaza nyota hao, Arsenal  iliwahi kujaribu kurusha karata yake kuwashawishi nyota wengine kama  Luis Suarez, Wayne Rooney na  Gonzalo Higuain,lakini ikashindwa na badala yake kocha  Wenger akajikuta akikaliwa kooni na mashabiki kwa kushindwa kutumia fedha msimu huu.

Mfaransa huyo tayari ameshaomba radhi kwa mashabiki kufuatia kipigo cha  Aston Villa aliwatumia ujumbe wa barua pepe uliosomeka: 

"Tunataka mashabiki wetu wawe na furaha. Unaposhindwa kufikia mafanikio hayo ni lazima ujihisi mnyonge na mwenye kuchanganyikiwa. Watu wanadhani hatutaki kutumia fedha ila tunataka kuzitumia."

No comments:

Post a Comment