STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, August 21, 2013

Hatimaye Abdi Kassim 'Babi' atua KMKM

Abdi Kassim 'Babi'
KIUNGO mshambuliaji nyota wa zamani wa Yanga na Taifa Stars, aliyekuwa akiichezea Azam katika Ligi Kuu Tanzania Bara msimu uliopita, Abdi Kassim 'Babi' au Ballack wa Ugunja' amemwaga wino wa kuichezea mabingwa wa Zanzibar KMKM.
Babi ambaye alikanusha taarifa za kutemwa na Azam na badala yake kueleza kwamba baada ya mkataba wake kumalizika aliamua kuachana na timu hiyo, ametgoa taarifa kupitia akaunti yake ya FB kwamba kwa sasa yeye ni mali ya KMKM baada ya kumwaga wino na kufurahi kupata nafasi ya kushiriki michuano ya kimataifa mwakani.
Mkali huyo aliyewahi kucheza soka la kulipwa Vietnam alisema kutua kwake KMKM kumempa faraja kutokana na kufanya kazi chini ya kocha mzoefu nchini, Ali Bushiri.
Ujumbe wake kwa mafans wake uliotumwa na mkali huyo mwenye mashuti makali unasomeka kama hivi hapo chini:
"Hi nyote ..Nashukuru Mungu mzima wa afya ..nimesaini mkataba na kmkm mabingwa wa soka zanzibar na timu inayo shiriki mashindano ya kimataifa na mashindano mbali mbal ..ikiongozwa na coach mzoefu na mwenye ujuzi wa hali ya juu..ali bushir .so natowa shukrani dha dhati kwa uwongozi wa kmkm kwa kumaliza soezi la usajil kati yangu.na wao na napenda kuwashukuru wote wapenzi wa kmkm ..kwa kuniunga mkono bamoja na uwongozi wa juu na nafurahi zaid kwa vile nipo nyumbani ..na famly yangu na biashara zangu za hapa na pale..asanten sana..watanzania wote .."
 

No comments:

Post a Comment