STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, August 21, 2013

Sifa zamtokea puani Diamond...Dk Mwakyembe ataka achunguzse ukaribu wake na 'wauza unga'

Diamond
BAADA ya msanii maarufu wa muziki wa kizazi kipya nchini Diamond Platnum kutajwa kujihusisha na mtandao wa dawa za kulevya waziri wa Uchukuzi Dk Harrison Mwakyembe atoa agizo msanii huyo aanze kuchunguzwa.
Msanii huyo leo ameripotiwa na baadhi ya vyombo vya habari kujihusisha na dawa za kulevya.
Uchunguzi huo utahusisha kuangalia vyanzo vyake vya mapato kama vinaendana na matumiz yake, wakati inasemekana  akaunti za diamond ambazo zinaonekana kubwa mno kulinganisha na kipato cha kawaida cha wasanii.
Hali hiyo imetokana na vugu vugu la kujaribu kuisafisha tanzania kutokana na kushamiri kwa madawa ya kulevya limefikia hatua nzuri na ya kipekee. Dk Mwakyembe amejitosa haswa kupambana na wauza unga, moja kati ya majina yanayosemekana ya wauza unga yanayodaiwa yapo ktk kitengo internal intelligency lipo jina la msanii Diamond.
Inasemekana Diamond ana urafiki wa karibu na mabosi wa Masogange, ambao wengine wapo nchini Afrika Kusini, kamera za cctv za uwanja wa wa ndege wa kitaifa JNIA zimekuwa zikionesha ukaribu wa Diamond na wale watu waliotajwa na Waziri Mwakyembe kuwa walimsaidia Masogange kupitisha mzigo.
Pia safari za kimuziki sehemu mbalimbali duniani ambazo nyingi hupangwa/kutafutwa na vigogo wa madawa ya kulevya waliopo tanzania na wale waliopo Afrika Kusini .
Wakati pia sasa serikali inajaribu kuchunguza akaunti za diamond ambazo zinaonekana kubwa mno kulinganisha na kipato cha kawaida cha wasanii. 
Uchunguzi bado unaendelea, lakini Diamond amekanusha kuhusika na sembe.
 
Chanzo:Pro24 

No comments:

Post a Comment