STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, August 9, 2013

PFA yamshushua Luis Suarez


LONDON, Uingereza
LIVERPOOL haifungwi kimkataba kumuuza Luis Suarez, kwa mujibu wa mwenyekiti wa chama cha wachezaji wa kulipwa (PFA), Gordon Taylor.
Suarez anaamini kwamba ana makubaliano na klabu hiyo ambayo yatamruhusu kujiunga na klabu inayoshiriki Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya, kama wataletewa ofa inayozidi paundi milioni 40.
Klabu hiyo ya Anfield imekataa ofa ya paundi milioni 40 na ziada ya paundi 1 kutoka kwa Arsenal, na Taylor amesema Liverpool walichoafiki ni kwamba watafanya tu mazungumzo na klabu husika kama ofa hiyo italetwa.
Taylor aliiambia Press Association: "Kama una kipengele cha kuvunjia mkataba ni lazima kieleze wazi, lakini hapa (kwa Suarez) ni tofauti kwa sababu kinasema kama Liverpool itashindwa kufuzu Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya na kama kuna ofa ya angalau paundi milioni 40 pande husika zitakaa mezani kujadili mambo lakini hakisemi kama klabu ni lazima imuuze.
"Iko wazi kwamba ofa ya paundi milioni 40 ndiyo kiwango awali cha kuanza mazungumzo, lakini inakuwa ngumu sana kwenye vipengele kama hivyo.
"Kuna kipengele cha 'maelewano ya kiungwana' katika suala 'siriasi' la mazungumzo ya uhamisho lakini siwezi kusema kinaibana Liverpool kwamba ni lazima imuuze.
"Luis ni mmoja wa memba wetu na tunataka kutoa sapoti yetu, hata hivyo, huenda anadhani kwamba ofa kama hiyo inaweza kulazimisha uhamisho."
Taylor pia alisema kwamba PFA itazungumza na Suarez na Liverpool katika jaribio la kulimaliza tatizo hilo.
Aliongeza: "Kwa sasa mambo hayako poa na sidhani kama ni hali nzuri kwa kila upande mchezaji au klabu zinazohusika.
"Hamna manufaa na ndiyo maana naona kwamba ni lazima tufanya kila tuwezalo tukae mezani na kuona kama kuna mazingira ya kufikiria uhamisho lakini kipengele kilichopo hakielezi wazi kwa asilimia 100.
"Tunawasiliana na pande zote kujaribu kuona kama suluhu itapatikana ambayo itazinufaisha pande zote."

No comments:

Post a Comment