STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, October 19, 2013

Huyu ndiye Wema Isaac Sepetu 'Beautiful Onyinye'

Wema Sepetu oct 2013 
Swali: Wema ni nani?
Jibu: Wema Sepetu is a girl, i can say a Lady mwenye umri wa miaka 24 kutoka familia ya Isack Abraham Sepetu, a darling, a libra.. a girl who is very ambicious, i love my self…

Swali: Siku yako ya kwanza shuleni ilikuaje?
Wema: Siku ya kwanza tumeenda nikakutana na msichana flani hivi anaitwa Shubira nakumbuka mpaka leo, alikua rafiki yangu wa kwanza tulikutana shuleni nilikua na miaka minne… tumekaa nikaanza kulia kwa sababu ilikua sehemu mpya, mazingira mapya baada ya hapo tukazoea.

Swali:Shule ilikua vipi kipindi unasoma?
Wema: Naweza kusema kipindi ambacho niko shule, Mwalimu wangu sijawahi kukaa hata siku moja kumfikiria mara mbili na haijawahi kutokea kwamba hata mwalimu akaweza kufanya labda matamanio au kutaka kitu chochote, hamna kitu kama hicho

Swali: Utafanya nini ikitokea umerudi shule?
Wema: Ningepata nafasi ya kurudi shule, academic nini uniform na nini… ningejaribu kuifanya more fun, a place where everybody can be just himself or herself and just be Wema Sepetu kwa sababu right now this is my time!!

Swali: Ni nani ambaye uko karibu nae kwenye familia yenu?
Wema: Dada yangu wa kwanza kuzaliwa anaitwa Tunu, tunakwenda sawa kwenye many many ways, kipindi mama yangu alivyonizaa aliumwa akalazwa hivyo dada yangu ndio akawa ananihudumia kama mtoto wake, ananinywesha uji… anahakikisha nimekunywa maziwa on time na mpaka leo ananiita my baby and I call her my mami… mtu wa pili ni dada yangu wa tatu, she is my bestfriend… baba yangu atabaki kuwa baba yangu tu, mama yangu ni my guardian Angel, my heart my darling.
Swali: Ulishawahi kugombana na ndugu zako?
Wema: Yeah nimegombana na dada yangu mpaka sasa hivi hatuongei, sio kitu chepesi….

Swali: Unaamini Mama yako ni mkorofi?
Wema: Linapokuja swala la mama yangu huwezi ukasema kwamba ni mkorofi lakini hapendi nikikosea wala kufanya kitu ambacho sicho…. kutokupenda kwake inafikia point anakua na hasira sana alafu njia ya kuonyesha hasira yake ndio level ya juu, yeye anafikiria kwamba anatengeneza ila badala ya kutengeneza ndio anaharibu.

Wema akiwa na mama yake
Swali: Wema ni mkorofi?
Wema: Mimi sio mkorofi, mtu ambae hanijui ndio ataniita mkorofi ukishanijua yani tutafika mbali lakini usiponijua na hujui ninachonitaka ndio tatizo.

Swali: Unajisikiaje kuwa Wema Sepetu?
Wema: Kuwa Wema Sepetu sio kitu rahisi, haiwezi kuwa kama watu wanavyofikiria  na haitakua hivyo kwa sababu ni maisha ambayo naishi, ni mpaka uone maisha ninayoishi ndio unielewe… yani hata kujaribu kuieleza ili uielewe napata tabu… mashabiki wangu wananielewa sana na uhusiano wangu na wao ni mzuri na ni tofauti na uhusiano kati yangu na familia yangu’

Swali: Unachukulia vipi unaposemwa ama kuandikwa vibaya?
Wema: Katika vitu vyangu ambavyo mtu wa nje anaweza kuviona kama vile… Mungu wangu Wema ana nini, mi navichukulia kama changamoto… mi naona kuna kitu special kuhusu mimi, kwa nini wasiseme watu wengine?

Swali: Unaamini wewe ni mrembo?
Wema: I am beautiful, naamini kwamba mimi ni beautiful kwa sababu nina pure heart… ni kitu Mwenyezi Mungu alichonibariki nacho.


Beautiful Onyinye, Wema Isaac Sepetu, Kuna maswali....?!

Swali: Kitu gani unachojivunia kwamba kinakutofautisha na wasanii wengine?
Wema: Ninachojivunia… uelewa wangu, I am very very smart.. ni mtu ambae ukiniambia kitu, fasta…. na hata kama sijui kitu, kujiua itanichukua muda mfupi, ability kusimama na kuongea na nikasikika, lugha…. hivyo ni vitu ambavyo najivunia sana

Swali: Unavuta sigara?
Wema: Ndio, ninapokua na msongo wa mawazo sana huwa nafanya hivyo  ili kuondoa mawazo na inaweza kutokea mara moja kwa mwezi.

Swali: Ni kweli kwamba wewe ni limbukeni wa umaarufu?
Wema: Sijaacha ustaa uniendeshe, unajua kuna wale watu wanaacha ustaa uwameze mpaka wanabadilisha kuongea, watu wengine wanaacha ule ustaa unawaendesha mwisho wa siku unaanza kuishi maisha ambayo hawana inafika point unaishi kama mtumwa mwisho wa siku unaishi maisha ambayo huna, unaanza kuumia Mungu wangu nimeshazoea kuishi maisha yale,  ishi vile ambavyo unaweza… huna pesa, huna! mimi ni mtu ambae ninaweza kuamka nasikia hamu ya kula mihogo, nafanya kitu ninachopenda na sio anachotaka mwingine’

Swali: Gucci na Vanny ni kina nani kwako?
Wema: My precious, kipenzi changu ni Vanny, katakufanya tu ukapende…. Gucci staa anajifanyaga kama yeye mtu tu wa kuchil!

Swali: Unaamini katika ushirikina?
Wema: Ushirikina najua kwamba upo, uchawi kama uchawi upo worldwide ila sipendi kujishirikisha manake sitaki siku moja kuwa mtumwa, mimi mtoto wa Kiislamu nafanya kisomo nachinja kila baada ya muda so naamini ukifanya hivyo unajikinga na vitu vingi.
Swali: Umeshawahi kurogwa?
Wema: Nimeshawahi kurogwa, imeshawahi kunitokea kabisa yani… ni kitu kingine ambacho huwa sipendi kukizungumzia.

Swali: Ulishawahi kwenda kwa Mganga?
Wema: Siwezi kuficha, wamekuja wengi ambao wanataka kunipeleka wengine mpaka kuniletea Waganga nyumbani kwangu lakini Quran mimi ndio mganga wangu namba moja.

Swali: Unafikiri kuna Wasanii wenzako ambao wanakuchukia?
Wema: Unategemea nini once ukishakua katika spotlight, hautegemei kuwa na watu wazuri karibu yako lazima wengine watakua ni wabaya na sio kila mmoja atakua anakuchekea kwa uzuri, wengine sio kutoka moyoni, wanakuchekea tu kwa sababu hawana choice.

Swali: Nani alikua mpenzi wako wa kwanza?
Wema: Sitaki kumtaja bwana….
wema na Diamond
Swali: Inasemekana unapenda mahusiano ya kimapenzi na watu maarufu?
Wema: Sio kwamba Wema anapenda kuwa na wapenzi maarufu, ni field ambayo tuko, tuko kwenye kiwanda kimoja kwa hiyo kwangu imekua iko hivyo, ni watu ambao mtakua mna interest zinaendana..

Swali: Umeshawahi kuwa na uhusiano wa kimapenzi na watu wangapi?
Wema: Wanne, watano au Wanaume sita hehhehe!!

Swali: Mlianza vipi mapenzi na Diamond?
Wema: Tulikua na hii Chemistry inaendana ilikua crazy, baada ya yeye kuniandikia msg kwenye facebook na kuniambia ananipenda, ni mtu ambae nilipata uzoefu mapenzi yanaweza kuwaje, nilipitia kwenye furaha na huzuni nikiwa na yeye…. kilichotokea kimetokea

Swali: Kuna ushindani wowote kati yako na Diamond?
Wema: Once upon a time kulikua na Diamond na Wema, na hawa watu walifall inlove…. watu wanajaribu sana kutulinganisha au tunaonekana tunashindana labda kwa sababu yeye anafanya vizuri kwenye industry yake na mimi nafanya vizuri kwenye industry yangu, mi sijawahi hata siku moja kushindana na Diamond…. mi kuimba siwezi.

Wema na Kajala
Swali: Kajala Masanja ni nani kwako?
Wema: Kajala ni rafiki, dada…. ndugu ambae hayuko kwenye ukoo wa Sepetu lakini uhusiano wangu na wake kwenye urafiki toka mwanzo sidhani kama nimewahi kuwa na uhusiano huu na mtu yeyote, watu wanadhani kwamba nimeanza kumjua juzi… tokea mwaka 2007 mi nimeanza kumfahamu Kajala mpaka tukawa marafiki sana hadi tunajikuta tumevaa sare.

Swali: Wazo la kumtolea Kajala dhamana ya milioni 13 lilitoka wapi?
Wema: Nilimuangalia Kajala analia pale kizimbani, aidha ilipwe faini au aende jela…. kilikua ni kitu ambacho hakijapangwa, ilikua suprise kwetu wote ila nilichokua nataka ni Kajala kuwa huru kwa hiyo kilichoweza kufanyika kilifanyika.

Wema wakati wa kesi yake iliyomalaza mahabusu
Swali: Ulijisikiaje siku tatu ulizolala Mahabusu?
Wema: Haikua nzuri kabisa, ni siku tatu mbaya kwenye maisha yangu… hakuna binadamu ambae hapendi uhuru, kwanini nilimsaidia Kajala na kupata nguvu ya kutoa hizo milioni 13? kwa sababu nimekuepo hapo… mimi siku tatu zilikua balaa sasa mwenzangu mwaka mmoja naa? ingekuaje? hata kama nisingemsaidia Kajala alafu Kajala ndio angekaa miaka hiyo 7 sijui 8 jela mimi nisingeweza kuishi, sio Wema Sepetu alivyo’

Swali: Best Werema ni nani katika kampuni yako?
Wema: Bestizzo ni blogger wangu na mpiga picha wangu, anarun kila kitu kinachohusu kampuni kwenye social network Website nini…

Swali: Kwanini uliamua kufanya nae kazi?
Wema: Kipindi cha kwanza niliona kumpa kazi ingeleta matatizo flani lakini nikafikiria, namjua Bestizzo alikua akifanya kazi kwa Diamond na alikua mfanyakazi mzuri, sijui ni kitu gani kilimfanya aondoke kwa Diamond kwa sababu mimi wakati sikua kwenye uhusiano mzuri na Diamond, Best bado alikua kwa Diamond na kipindi hicho hata bado nilikua sijafungua kampuni, hata alikua haniombi kazi ila alihitaji nimuunganishe na wengine’

Wema akiwa na Kadinda
Swali: Uko vipi na Tinny Dad, Pettman na Martin Kadinda?
Wema: Tiny na Petti ni watu wangu wa karibu sana, nimewajua kwa muda mrefu na wananijua na ninawajua.. Kadinda kabla ya kuwa meneja wangu alikua rafiki yangu, hakua rafiki yangu wa hivyo… tulikua hatuonani hata miezi sita lakini tukikutana namwambia yote yaliyopita, mwaka juzi ndio Martin akasema ngoja niwe Meneja wako, hatukua hata na mikataba mwanzoni… tukajaribisha na tukafanikiwa mpaka leo niko nae.


credit: millardayo

No comments:

Post a Comment