STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, October 19, 2013

Akina Samatta, Ulimwengu watinga Fainali Afrika

Mbwana Samatta atacheza Fainali ya Kombe la Shirikisho na timu yake ya TP Mazembe

Kikosi cha TP Mazembe kilichotangulia fainali za Kombe la Shirikisho Afrika
WASHAMBULIAJI nyota wa Tanzania, Mbwana Samatta na Thomas Ulimwengu wameweka rekodi baada ya timu yao ya TP Mazembe ya DR Congo kutinga hatua ya Fainali za Kombe la Washindi Afrika kutokana na ushindi wa bao 1-0 iliyopata jioni hii dhidi ya Stade Malien Bamako mjini Lubumbashi.
Bao pekee lililoipeleka fainali TP Mazembe na kuwafanya watanzania hao kuingia katika rekodi ya kukaribia kuwa Watanzania wa kwanza kunyakua taji kubwa barani Afrika, liliwekwa kimiani na Tresor Mputu kwa njia ya penati katika dakika ya 7 tu ya mchezo huo.
Kwa ushindi hio TP Mazembe imefuzu fainali kwa jumla ya mabao 3-1 baada ya mechi ya awali iliyochezwa mjini Bamako, Mali kushinda mabao 2-1.
Mabingwa hao wa zamani wa Afrika wanasubiri kujua itacheza na nani katika fainali ya michuano hiyo kati ya timu mbili za Tunisia, CA Bizertin itakayovaana na CSSfaxien kesho katika pambano la marudiano huku matokeo ya mechi ya kwanza yakiwa 0-0.

No comments:

Post a Comment