STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, October 19, 2013

Kun Aguero aizamisha West Ham, Manchester City ikiua x3

Sergio 'Kun' Aguero

MABAO mawili ya mshambuliaji nyota wa Argentina, Sergio 'Kun' Aguero, yalitosha kuisaidia Manchester City kuizamisha West Ham kwa mabao 3-1 katika pambano lililomalizika hivi punde la Ligi Kuu ya England.
Wakiwa ugenini, Manchester City waliwashtua wenyeji wao kwa kupata bao la kuongoza lililofungwa katika dakika ya 16 kupitia Kun Aguero na kudumu hadi wakati wa mapumziko.
Kipindi cha pili kilishiuhudia  Kun Aguero akiiongezea timu yao bao la pili dakika sita tu tangu kipindi hicho kianze kabla ya wenyeji West Ham kupata bao la kujifutia machozi kupitia kwa Ricardo Vaz Te dakika ya 58.
David Silva aliihakikishia Man City ushindi kwa kufunga bao la tatu dakika 10 kabla ya kumalizika kwa pambano hilo na kuifanya ichupe hadi nafasi ya nne katika msimamo wa ligi hiyo ikifikisha pointi 16 ikiwa nyuma ya timu ya Liverpool na Chelsea waliopo juu yao wakiifukuzia Arsenal inayoongopa baada ya jioni ya leo kupata ushindi mnono wa mabao 4-1 wakiwa nyumbani Emirates.

No comments:

Post a Comment