STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, October 19, 2013

Yanga watua Dar na matumaini kibao kuinyuka Simba kesho


MABINGWA watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Yanga imetua jijini Dar es Salaam leo ikitokea visiwani Pemba ilipoenda kuweka kambi kujiandaa na pambano lao la kesho dhidi ya Simba na kuapa 'mnyama' lazima afe kesho Taifa.
Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa na mtandao wa klabu hiyo ya Yanga zinasema kuwa kikosi kamili cha mabingwa hao watetezi kimetua leo kikiwa na matumaini kibao ya kumchinja mnyama kesho katika pambano la kwanza la wapinzani hao wa jadi kwa msimu huu.
Taarifa hiyo inasema Yanga ilijifua asubuhi ya leo kabla ya kurejea jijini ikiwa ni maandalizi ya mwisho mwisho kwa ajili ya pambano hilo na kwamba kocha Ernie Brandts alisema hakuna mchezaji yeyote mgonjwa hali inayompa matumaini ya kucheka kesho.
"Sisi tumejiandaa vizuri kwa ajili ya mchezo huo, vijana wangu wapo safi kiafya, kifikra na morali ni ya hali ya juu, hivyo tuna kila sababu ya kuendeleza wimbi la ushindi ukizingatia uwezo wa kikosi chetu kwa ujumla hivi sasa" alinukuliwa Brandts Aidha Brandts alisema anatambua michezo ya watani wa jadi duniani kote huwa ni migumu lakini kwa sasa haoni sababu itakayowazuia kuibuka na ushindi katika mchezo huo japokuwa Simba timu nzuri pia.
Ushindi kwetu siku ya jumapili ni muhimu, ni muhimu kwa sababu tunapigania kutetea tena ubingwa wetu kwa awamu ya pili mfululizo, kikubwa tunawaomba wapenzi, washabiki na wanachama waje kwa wingi kuwashangilia vijana wao watakpokuwa wanapeperusha bendera ya watoto wa Jangwani.

No comments:

Post a Comment