STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, October 19, 2013

Simba ina nafasi kubwa kuitungua Yanga kesho, japo...!

Heka heka za Simba na Yanga

INGAWA viongozi na hata wanachama na mashabiki wa Yanga wana imani kubwa kwa timu yao kuibuka na ushindi kesho katika pambano la watani wa jadi linalofanyika kwenye uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, bado mabingwa watetezi hao wanapaswa kuwa makini kwani Simba ina nafasi kubwa zaidi ya kuiangusha Yanga.
Yanga wanaamini wana kikosi imara na kinachoweza kuwazima mapema Simba inayonolewa na kocha King Abdallah Kibadeni, lakini kwa mashabiki wa soka wanaofuatilia mechi za watani wa jadi bado Yanga ina kazi kubwa kwa Simba hata kama wanaonekana siyo imara zaidi ya vijana wa Jangwani.
Kama nilivyomnukuu winga wa zamani wa timu ya Yanga na TAMCO-Kibaha aliyewahi kuwa Katibu Mkuu wa Chama cha Soka Wilaya ya Kinondoni (KIFA) Ramadhani Kampira Yanga wasipokuwa makini huenda kesho wakakoga kipigo bila kutarajia na kuleta mtafaruku mkubwa klabuni kwao.
Unajua kwanini?
Rekodi zinaonyesha kuwa wakati Yanga inapokuwa ikonekana kuwa imara na bora ndipo wanapoadhiriwa na Simba, kadhalika Simba inapoonekana kuwa ngangari zaidi huishia kuumia kwa watani zao hao.
Zipo baadhi ya mechi ambazo ukizifuatilia baina ya timu hizo zinaonyesha wakati klabu moja ikiwa juu kisoka na kuundwa na wachezaji wakali ndipo ilipokuwa aikiibishwa na ile iliyoonekana nyonge kuibuka kidedea.
Kwa mfano pambano baina ya timu hizo mwaka Julai 1988, Yanga ikihitaji sare ili kutwaa ubingwa na Simba iliyokuwa chovu ikisaka ushindi ili isihuke daraja, nini kilitokea? Yanga ililala kwa mabao 2-1.
Orodha ya mechi hizo ni ndefu lakini kwa uchache kuanzia miaka ya 1990 mpaka sasa utagundua ukweli huu na kinachosababisha kutokea kwa hali hiyo ni upande unaojiona bora na imara kujiamini kupita kiasi na mwishowe kukumbana na matokeo wasiyotarajiwa uwanjani kitu kinachoweza kuikuta Yanga kesho.
Kwa mfano hivi sasa Yanga inaoonekana kujiamini kupita kiasi hadi kufikia wanachama na wazee wa klabu hiyo kutangaza kwamba wataitungua Simba mabao 3-0, lakini wanasahau kuwa Simba siyo timu ya kubeza na inanolewa na makocha wenye kujua fitina za Simba na Yanga kwa ufasaha zaidi wakiwa wenyewe wameshawahi kucheza mechi za wapinzani hao enzi zao za uchezaji.
Kibadeni na msaidizi wake na hata kocha wa makipa, James Kisaka wanajua 'in and out' ya fitina za mechi za Simba na Yanga kulinganisha na Brandts na wasaidizi wake wengine ukimuondoa Fred Felix Minziro.
Sidhani kama Kibadeni na Julio watapenda kuadhiriwa na Yanga katika mechi ya kesho uwanja wa Taifa, ikizingatiwa kuwa kipigo chochote kwao kitawaondoa kileleni na kuwapisha watani zao kuwatangulia kutegemea na idadi ya mabao watakayofungwa.
Pia, imani yangu makocha hao watawajaza upepo wachezaji wao kupigana kiume ili kumbeba katika pambano hilo na kujihakikishia nafasi katika kikosi mbele ya Kibadeni ambaye huwa haangalii ukubwa wa jina la mchezaji zaidi ya nidhamu, kujituma uwanjani na mazoezini na namna ya kuisaidia timu.
Aina na wastani wa umri wa wachezaji waliopo Simba kulinganisha na Yanga unaweza kubaini kuwa Simba wana nafasi kubwa ya kuwapeleka Yanga mchakamchaka dimbani, iwapo tu wachezaji hao wa Simba watazingatia maelekezo ya walimu wao sambamba na kuonyesha vipaji vyao halisi walivyonavyo.
Kadhalika ipo imani iliyojengeka na kuaminika kwa wengi na hata wana Msimbazi wenyewe kwamba siku ya Jumapili ni SIKU YAO kama ilivyo kwa Yanga wanaoamini mechi ikichezwa JUMAMOSI asimilia zote kushinda ni LAZIMA.
Hata hivyo kwa vile soka halipo hivyo kwa kuangalia imani na historia ni vyema tusubiri tuone hiyo kesho kati ya vijana wa Jangwani na Msimbazi nani watakaolala mapema kwa aibu na wapi watakaokesha kwa furaha kushangilia ushindi?
Chini ni orodha ya mechi za watani hao wa jadi katika michuano ya Ligi tangu mwaka 1965 hadi Mei, 2013
JUNI 7, 1965
Yanga v Sunderland (Simba)
1-0
MFUNGAJI: Mawazo Shomvi dk. 15).

JUNI 3,  1966
Yanga v Sunderland (Simba)
3-2
WAFUNGAJI:
Yanga: Abdulrahman Lukongo dk. 54, Andrew Tematema dk 67, Emmanuel Makaidi dk. 83. Sunderland: Mustafa Choteka dk 24, Haji Lesso dk. 86.

NOVEMBA 26, 1966
Sunderland v Yanga
1-0
MFUNGAJI: Mustafa Choteka dk. 44.

MACHI 30, 1968
Yanga v Sunderland
1-0
MFUNGAJI: Kitwana Manara dk. 28.

JUNI 1, 1968
Yanga v Sunderland
5-0
WAFUNGAJI:
Maulid Dilunga dk. 18 (penalti), Dilunga dk. 43, Salehe Zimbwe dk. 54, Zimbwe dk. 89, Kitwana Manara dk. 86.

MACHI 3, 1969
Yanga v Sunderland
(Yanga ilipewa pointi za chee na ushindi wa mabao 2-0, baada ya Sunderland kugoma kuingia uwanjani).

JUNI 4, 1972
Yanga v Sunderland
1-1
WAFUNGAJI:
Yanga: Kitwana Manara dk. 19,
Sunderland: Willy Mwaijibe dk. 11.

JUNI 18, 1972
Yanga v Simba
1-0
MFUNGAJI: Leonard Chitete.

JUNI 23,  1973
Simba v Yanga
1-0
MFUNGAJI: Haidari Abeid 'Muchacho' dk. 68.

AGOSTI 10, 1974
Yanga v Simba
2-1
WAFUNGAJI:
Yanga: Gibson Sembuli dk. 87, Sunday Manara dk. 97.
Simba: Adam Sabu dk. 16.
(Mechi ya kihistoria iliyochezwa Uwanja wa Nyamagana mjini Mwanza).

JULAI 19, 1977
Simba v Yanga
6-0
WAFUNGAJI:
Abdallah Kibadeni dk. 10, 42 na 89, Jumanne Hassan 'Masimenti' dk. 60 na 73, Selemani Sanga alijifunga dk. 20.

OKTOBA 7, 1979
Simba v Yanga
3-1
WAFUNGAJI:
Simba: Nico Njohole dk. 3, Mohammed Bakari 'Tall' dk. 38, Abbas Dilunga dk.72. Yanga: Rashidi Hanzuruni dk. 4.

OKTOBA 4, 1980
Simba v Yanga
3-0
WAFUNGAJI: Abdallah Mwinyimkuu dk. 29, Thuwein Ally dk. 82, Nico Njohole dk. 83.

SEPTEMBA 5, 1981
Yanga v Simba
1-0
MFUNGAJI: Juma Hassan Mkambi dk. 42

APRILI 29, 1982
Yanga v Simba
1-0
MFUNGAJI: Rashid Hanzuruni dk 2.

SEPTEMBA 18, 1982
Yanga 3-0 Simba
WAFUNGAJI:
Omar Hussein dk. 2 na 85, Makumbi Juma dk. 62.

FEBRUARI 10, 1983
Yanga v Simba.
0-0

APRILI 16, 1983
Yanga v Simba
3-1
WAFUNGAJI:
Yanga: Charles Mkwasa dk. 21, Makumbi Juma dk. 38, Omar Hussein dk. 84, Simba; Kihwelu Mussa dk. 14.

SEPTEMBA 10, 1983,
Yanga v Simba
2-0
WAFUNGAJI: Lila Shomari alijifunga dk. 72, Ahmed Amasha dk. 89.

SEPTEMBA 25, 1983
Yanga v Simba
1-1
WAFUNGAJI:
Yanga: Makumbi Juma dk. 75,
Simba: Sunday Juma dk. 72.

MACHI 10, 1984
Yanga v Simba
1-1
WAFUNGAJI:
Yanga: Omar Hussein dk. 72.
Simba: Idd Pazi kwa penalti dk 20.

JULAI 14, 1984
Yanga v Simba
1-1
WAFUNGAJI:
Yanga: Abeid Mziba dk. 39.
Simba: Zamoyoni Mogella dk. 17

MEI 19, 1985
Yanga v Simba
1-1
WAFUNGAJI:
Yanga: Omar Hussein dk. 6
Simba: Mohammed Bob Chopa dk. 30.

AGOSTI 10, 1985
Yanga v Simba
2-0

MACHI 15, 1986
Yanga v Simba
1-1
WAFUNGAJI:
Yanga: Abeid Mziba dk. 44
Simba: John Hassan Douglas dk. 20.

AGOSTI 23, 1986
Simba v Yanga
2-1
WAFUNGAJI:
Simba: Edward Chumila dk. 9, Malota Soma dk. 51
Yanga: Omar Hussein dk. 5.

JUNI 27, 1987
Yanga v Simba
1-0
MFUNGAJI: Edgar 'Fongo' Mwafongo dk. 36.

AGOSTI 15, 1987
Yanga v Simba
1-0
MFUNGAJI: Abeid Mziba dk. 14.

APRILI 30, 1988
Yanga v Simba
1-1
WAFUNGAJI:
Yanga: Justin Mtekere dk. 28
Simba: Edward Chumila dk. 25.

JULAI 23, 1988
Simba v Yanga
2-1
WAFUNGAJI:
Simba: Edward Chumila 21, John Makelele dk. 58
Yanga: Issa Athumani dk. 36.

JANUARI 28, 1989
Yanga v Simba
2-1
WAFUNGAJI:
Yanga: Issa Athumani dk. 4, Abeid Mziba dk. 85
Simba: Malota Soma dk. 30.

MEI 21, 1989
Yanga v Simba
0-0

MEI 26, 1990
Simba v Yanga
1-0
MFUNGAJI: Mavumbi Omari dk 6.

OKTOBA 20, 1990
Yanga v Simba
3-1
WAFUNGAJI:
Yanga: Makumbi Juma dk 33, Thomas Kipese dk. 82, Sanifu Lazaro dk. 89
Simba: Edward Chumila dk. 58.

MEI 18, 1991
Yanga v Simba
1-0
MFUNGAJI: Said Sued 'Scud' dk.  7.

AGOSTI 31, 1991
Yanga v Simba
1-0
MFUNGAJI: Said Sued Scud.

OKTOBA 9, 1991
Yanga v Simba
2-0
WAFUNGAJI: Athumani China dk. 3, Abubakar Salum 'Sure Boy' dk. 54.

NOVEMBA 13, 1991
Yanga v Simba
2-0

APRILI 12, 1992
Yanga 1-0 Simba
MFUNGAJI: Kenneth Mkapa dk. 10.

SEPTEMBA 26, 1992
Simba v Yanga
2-0

OKTOBA 27, 1992
Simba v Yanga
1-0
MFUNGAJI: Damian Morisho Kimti.

MACHI 27, 1993
Yanga v Simba
2-1
WAFUNGAJI:
Yanga: Said Mwamba Kizota dk. 47 na 57
Simba: Edward Chumila dk. 75.

JULAI 17, 1993
Simba v Yanga
1-0
MFUNGAJI: Dua Said dk. 69.

SEPTEMBA 26, 1993
Simba v Yanga
1-0
MFUNGAJI: Dua Said dk. 13.

NOVEMBA 6, 1993
Simba v Yanga
0-0

FEBRUARI 26, 1994
Yanga v Simba
2-0
MFUNGAJI: Mohammed Hussein 'Mmachinga' na James Tungaraza 'Boli Zozo'.

JULAI 2, 1994
Simba v Yanga
4-1
WAFUNGAJI:
Simba: George Masatu, Athumani China, Madaraka Selemani, Dua Saidi Yanga; Constantine Kimanda.

NOVEMBA 2, 1994
Simba v Yanga
1-0
MFUNGAJI: Madaraka Selemani dk. 71

NOVEMBA 21, 1994
Simba v Yanga
2-0
WAFUNGAJI: George Lucas dk. 18, Madaraka Selemani dk. 42.

MACHI 18, 1995
Simba v Yanga
0-0

OKTOBA 4, 1995
Simba v Yanga
2-1
WAFUNGAJI:
Simba: Said Mwamba 'Kizota' dk. 70, Mchunga Bakari dk. 79,
Yanga: Mohamed Hussein ÔMmachingaŐ dk. 40.

FEBRUARI 25, 1996
Yanga v Simba
2-0

SEPTEMBA 21, 1996
Yanga v Simba
0-0

OKTOBA 23, 1996
Yanga v Simba
1-0
MFUNGAJI: Mohamed Hussein 'Mmachinga' dk. 46

NOVEMBA 9, 1996
Yanga v Simba
4-4
WAFUNGAJI:
Yanga: Edibilly Lunyamila (penalti) dk. 28, Mustafa Hozza alijifunga dk 64, Said Mwamba 'Kizota' dk. 70, Sanifu Lazaro dk. 75.
Simba: Thomas Kipese dk. 7, Ahmed Mwinyimkuu dk. 43, Dua Saidi dk. 60 na 90.
(Mechi hii ilichezwa Uwanja wa Sheikh Amri Abeid mjini Arusha)

APRILI 26, 1997
Yanga v Simba
1-1
WAFUNGAJI:
Yanga: Idelfonce Amlima dk. 16
Simba: Abdallah Msamba sekunde ya. 56

AGOSTI 31, 1997
Yanga v Simba
0-0

OKTOBA 11, 1997
Yanga v Simba
1-1
WAFUNGAJI:
Yanga: Sekilojo Chambua dk. 52
Simba: George Masatu dk. 89
(Mechi hii ilichezwa Uwanja wa Sokoine mjini Mbeya)

NOVEMBA 8, 1997
Yanga v Simba
1-0
MFUNGAJI: Sekilojo Chambua dk. 85
(Mechi hii ilichezwa Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma)

FEBRUARI 21, 1998
Yanga v Simba
1-1
WAFUNGAJI:
Yanga: Akida Makunda dk. 46
Simba: Athumani Machepe dk. 88

JUNI 7, 1998
Yanga v Simba
1-1
WAFUNGAJI:
Yanga: Idelfonce Amlima dk. 28
Simba: Abuu Juma (penalti) dk. 32

MEI 1, 1999
Yanga v Simba
3-1
WAFUNGAJI:
Yanga: Idd Moshi dk. 59, Kalimangonga Ongala dk. 64, Salvatory Edward dk. 70, Simba: Juma Amir dk. 12.

AGOSTI 29, 1999
Yanga v Simba
2-0
WAFUNGAJI: Bakari Malima dk. 49, Mohamed Hussein 'Mmachinga' dk 71

JUNI 25, 2000
Simba v Yanga
2-1
WAFUNGAJI:
Simba: Steven Mapunda dk. 59 na 72
Yanga: Idd Moshi dk. 4.

AGOSTI 5, 2000
Yanga v Simba
2-0
MFUNGAJI: Iddi Moshi 37 na 47. (Alifunga mabao hayo, akitoka kwenye fungate ya ndoa yake)

SEPTEMBA 1, 2001
Simba v Yanga
1-0
MFUNGAJI: Joseph Kaniki dk. 76

SEPTEMBA 30, 2001
Simba v Yanga
1-1
WAFUNGAJI:
Simba: Joseph Kaniki dk. 65,
Yanga: Sekilojo Chambua dk. 86
(Mechi hii ilichezwa Uwanja wa CCM Kirumba mjini Mwanza)

AGOSTI 18, 2002
Simba v Yanga
1-1
WAFUNGAJI:
Simba: Madaraka Selemani 65
Yanga: Sekilojo Chambua (penalti). dk. 89

NOVEMBA 10, 2002
Simba v Yanga
0-0

SEPTEMBA 28, 2003

Simba v Yanga
2-2
WAFUNGAJI:
Simba: Emmanuel Gabriel dk. 27 na 36
Yanga: Kudra Omary dk. 42, Heri Morris dk. 55

NOVEMBA 2, 2003
Simba v Yanga
0-0

AGOSTI 7, 2004
Simba v Yanga
2-1
WAFUNGAJI:
Simba: Shaaban Kisiga dk. 64, Ulimboka Mwakingwe dk. 76
Yanga: Pitchou Kongo dk. 48

SEPTEMBA 18, 2004
Simba v Yanga
1-0
MFUNGAJI: Athumani Machuppa dk. 82

APRILI 17,  2005
Simba v Yanga
2-1
WAFUNGAJI:
Simba: Nurdin Msiga dk. 44, Athumani Machupa dk. 64,
Yanga: Aaron Nyanda dk. 39
(Mechi hii ilichezwa Uwanja wa Jamhuri, Morogoro)

AGOSTI 21, 2005
Simba v Yanga
2-0
MFUNGAJI: Nico Nyagawa dk. 22 na 56
(Mechi hii ilichezwa Uwanja wa Sheikh Amri Abeid mjini Arusha)

MACHI 26, 2006
Simba v Yanga.
0-0

OKTOBA 29, 2006
Simba v Yanga
0-0

JULAI 8, 2007
Simba v Yanga
1-1 (dakika 120)
WAFUNGAJI:
Simba: Moses Odhiambo (penalti dk. 2)
Yanga: Said Maulid (dk. 55).
(Simba ilishinda kwa mikwaju ya penalti 5-4 baada ya sare hiyo).
(Mechi hii ilichezwa Uwanja wa Jamhuri, Morogoro)

OKTOBA 24, 2007:
Simba Vs Yanga
1-0
Mfungaji: Ulimboka Mwakingwe
(Mechi hii ilichezwa Uwanja wa Jamhuri, Morogoro)

APRILI 27, 2008:
Simba Vs Yanga
0-0

OKT 26, 2008
Yanga Vs Simba
1-0
MFUNGAJI: Ben Mwalala dk15.
(Mechi hii ilichezwa Uwanja mpya wa Taifa, Dar es Salaam)

APRILI  19, 2009
Simba Vs Yanga
2-2
WAFUNGAJI:
SIMBA: Ramadhan Chombo dk 23, Haruna Moshi dk 62
YANGA: Ben Mwalala dk48, Jerry Tegete dk90
(Mechi hii ilichezwa Uwanja mpya wa Taifa, Dar es Salaam)

OKTOBA 31, 2009
Simba Vs Yanga
1-0
MFUNGAJI: Mussa Hassan Mgosi dk 26
(Mechi hii ilichezwa Uwanja mpya wa Taifa, Dar es Salaam)

APRILI 18, 2010
Simba Vs Yanga
4-3
WAFUNGAJI:
SIMBA: Uhuru Suleiman dk 3, Mussa Mgosi dk 53 na 74, Hillary Echesa dk 90+
YANGA: Athumani Iddi dk 30, Jerry Tegete dk 69 na 89

OKTOBA 16, 2010:
Yanga Vs Simba
1-0
MFUNGAJI: Jerry Tegete dk 70

MACHI 5, 2011
Simba Vs Yanga
1-1
WAFUNGAJI:
YANGA: Stefano Mwasyika (penalti) dk 59.
SIMBA:  Mussa Mgosi dk 73.

OKTOBA 29, 2011
Yanga 1-0 Simba
MFUNGAJI: Davies Mwape dakika ya 75


MEI 6, 2012
Simba 5-0 Yanga
WAFUNGAJI:
Emmanuel Okwi dk 1 na 65, Patrick Mafisango pen dk 58, Juma Kaseja pen dk 69 na Felix Sunzu pen dk 74.

OKT 3, 2012
Yanga 1-1 Simba
WAFUNGAJI:
SIMBA: Amri Kiemba dk 3,
YANGA: Said Bahanuzi dk 64

MEI 6, 2013
Simba 0-2 Yanga
WAFUNGAJI:  Didier Kavumbagu dk 5 na Hamis Kiiza dk 62

No comments:

Post a Comment