STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, October 19, 2013

Liverpool chupuchupu kwa Newcastle, Gerrard afunga la 100 EPL

Liverpool striker Daniel Sturridge heads in a goal against Newcastle
Sturridge akisawazisha bao la pili la Liverpool (Picha:BBC Sport)

NEWCASTLE United ikiwa dimba lake la nyumbani ya St Jamed Park ikicheza pungufu ya mchezaji mmoja kwa dakika 50, imeing'ang'ania Liverpool na kulazimisha sare ya mabao 2-2, wageni wakichomoa mara mbili ili kuambulia sare hiyo iliyowapeleka kileleni kwa muda kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya England ikifikisha pointi 17, moja zaidi ya Arsenal itakayokuwa nyumbani kuialika Norwich City jioni hii.
Beki Yanga Mbiwa alijikuta akilimwa kadi nyekundu katika dakika ya 40 ya mchezo huo baada ya kumwamgusha Luis Suarez aliyekuwa akienda kumsalimia kipa wake Tim Krul wakati Newcastle ikiwa mbele kwa bao 1-0.
Kosa hilo la Yanga-Mbiwa, lilisababisha Liverpool kupata penati iliyotumbukizwa wavuni katika dakika ya 42 na nahodha Steven Gerrard, likiwa ni bao lake la 100 katika Ligi Kuu ya England.
Kabla ya Gerrard kupata bao hilo la kusawazisha, awali Newcastle ilikuwa mbele kwa bao lililofungwa na Yohan Cabaye katika dakika ya 23 akimalizia kazi nzuri ya Cheikh Tiote.
Kipindi cha pili kilianza kwa kasi na wenyeji kujipatia bao la pili dakika ya 57 kupitia Paul Dummett , lakini katika dakika ya 72 mfungaji anayoongoza kwa kufumani nyavu kwa sasa EPL, Daniel Sturridge aliiepushia aibu Liverpool kwa kufunga bao la pili la kusawazisha na matokeo hayo kudumu hadi mwisho wa mchezo.
Hata hivyo Liverpool itakaa kwa muda kileleni kwani mechi mbalimbali zinaendelea kuchezwa jioni hii ambapo tayari Arsena wanaoongoza kwa bao 1-0 dhidi ya wageni wao Norwich, bao likifungwa na Jack Wilshere.

No comments:

Post a Comment