STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, October 19, 2013

Mdogo wa Super Nyamwela akwaa kashfa nzito


Juma Nyamwela (nyuma) anayedaiwa kulawiti mtoto

MNENGUAJI wa kiume wa Mashujaa Band, Juma Nyamwela (Nyamwela Jr) amekamatwa na polisi kwa tuhuma za kumlawiti mtoto wa kiume wa umri wa miaka sita.

Kwa sasa mnenguaji huyo yupo kituo cha polisi cha Mabatini Kijitonyama jijini Dar es Salaam ikiwa ni siku ya tatu tangu akamatwe kwa tuhuma hizo.

Habari za uhakika kutoka kituoni hapo zinasema katika maelezo ya awali, mnenguaji huyo amekiri kosa.

Chanzo cha Chetu kimeeleza kuwa huenda mnenguaji huyo akafikishwa mahakamani siku ya Jumatatu.
Nyamwela Jr (wa tatu toka kulia) akiwa na wasanii wenzake wa Mashujaa
 Nyamwela ambaye ni mdogo wake na Super Nyamwela wa Extra Bongo, aliwahi kuitumikia TOT Plus kabla ya kujiunga na Mashujaa Band. 

Mwaka 2007 aliibuka bingwa wa mashindano ya dansa bora wa kiume yaliyoandaliwa na Usher Family na kujinyakulia zawadi ya gari.

Source:- Salute5

No comments:

Post a Comment