STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, October 19, 2013

AS Roma yaizima Napoli 2-0

Mfungaji wa mabao yaliyoizamisha Napoli, Miralem Pjanic

KLABU ya AS Roma usiku wa kuamkia leo iliweza kukwea kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu ya Italia Seria A baada ya kuwanyuka Napoli kwa mabao 2-0, mjini Roma.
Mabao mawili ya Miralem Pjanic yalitosha kuzima ubabe wa Napoli ambayo ilikuwa haijapoteza mechi yoyote katika ligi hiyo.
Mfungaji huyo alifunga mabao hayo katika dakika za nyongeza kabla ya kumalizika kwa kipindi cha kwanza na jingine la mkwaju wa penati dakika ya 71 yalifanya Roma kukaa kileleni ikiwa imejikusanyia jumla ya pointi 24, na kuiporomosha Napoli hadi nafasi ya tatu ikiipisha Juventus wanaolingana nao pointi 19 kushika nafasi ya pili.
Juventus leo inatarajiwa kushuka dimbani leo ugenini kuumana na Fiorentina katika mfululizo wa ligi hiyo, ambapo hata kama itapata ushindi bado haijaweza kuwaondoa Roma kileleni.

No comments:

Post a Comment