STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, October 20, 2013

Msiba! Mtangazaji Julius Nyaisanga 'Uncle J' hatunaye


Julius Nyaisanga enzi za uhai wake
TAARIFA zilizotufikia kutokana Morogoro zinasema kuwa, Mtangazajai nguli aliyewahi kutamba na vituo mbalimbali vya Radio kuanzia RTD, Radio One/ITV, Julius Nyaisangah 'Uncle J' amefariki dunia kutokana na kuugua kwa muda mrefu akiwa hospitali ya Mazimbu mjini humo.
Marehemu Nyaisanga anayekumbukwa kwa umahiri wake wa kutangaza taarifa habari na kuendesha vipindi vya Misakato na Klabu Raha Leo Show wakati yupo RTD na kisha kutisha na Mambo Mseto na Watoto Show akifahamika kama Babu wa Kimazichana akiwa Radio One, mpaka mauti yanamkumba alikuwa Mhairir Mtendaji wa Abood Media inayomiliki vituo vya Radio Abood na Abood Televisheni za mjini Morogoro.
Haijafahamika chanzo halisi cha mauti ya mtangazaji huyo, japo inaelezwa alikuwa akiigua kwa muda mrefu kisukari na Shinikizo la damu.
MICHARAZO inatoa pole kwa ndugu, jamaa na familia ya marehemu pamoja na wadau wote wa tasnia ya habari na kuwatakia subira katika kipindi hiki kigumu cha msiba.
Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema  Ameen

No comments:

Post a Comment