STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, October 20, 2013

Polisi Dar wanasa wamwagia tindikali

 
Kamanda Kova
JESHI la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam linawashikilia watu wawili kwa tuhuma za kujihusisha na matukio ya kumwagia watu kemikali aina ya tindikali.
Watuhumiwa hao ambao hata hivyo hawakutajwa majina, walikamatwa Oktoba 10, mwaka huu saa 2:00 asubuhi katika maeneo ya Lumumba, Kariakoo.
Akizungumza na waandishi wa habari jana ofisini kwake, Kamishna wa Polisi, Kamanda wa Kanda hiyo Suleiman Kova alisema, watuhumiwa hao walikiri kuhusika na tukio moja la kummwagia mfanyabiashara Ally Farhat (33) ambaye ni raia wa Lebanon, tukio ambalo liliripotiwa katika Kituo cha Polisi Msimbazi.
"Taarifa za kiintelejensia zinaonesha mbinu zilizotumika katika tukio hilo zinawiana na tukio la kumwagiwa sumu aina ya tindikali mfanyabiashara aitwaye Said Mohamed maarufu kama Saad (42) ambaye ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Home Shopping Center (HSC), tukio ambalo lilifanyika maeneo ya Msasani katika jengo la Msasani City Mall mwezi Julai, mwaka huu," alisema Kamanda Kova.
Hata hivyo Kamanda Kova hakutaka kuwataja majina yao kutokana na kile alichosema bado wanaendelea kuwahoji hivyo wanahofia kupoteza ushahidi endapo majina hayo yatawekwa wazi.
Aidha alisema pia wanaendelea kuwahoji ili kubaini ushiriki wao katika tukio hilo, pia wanashirikiana na mikoa ya Zanzibar na mikoa mingine ili kubaini kama walishiriki katika matukio ya aina hiyo.
Aidha katika tukio jingine Kamanda Kova alisema, wamefanikiwa kumkamata mtuhumiwa mmoja Raia wa Somali aitwaye Jamal Ibrahim (42) akiwa na nyaraka za Serikali zikiwemo stakabadhi za malipo ya vibali vya makazi.
Kamanda Kova alitaja vitu alivyokutwa navyo mtu huyo kuwa ni pamoja na fomu namba 130 za maombi ya makazi, stakabadhi 21 za malipo ya vibali vya makazi, nakala nane za hati za kusafiria zenye picha za waombaji ambao ni raia wa Somalia na bahasha moja yenye picha mbalimbali za waombaji ambao ni raia wa Somalia.

No comments:

Post a Comment