STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, October 20, 2013

Monaco washindwa kurejea kileleni Ligue 1 yabanwa na Sochaux



LICHA ya kutangulia kupata mabao mawili ya haraka na kuongoza kwa muda mrefu, Monaco imeshindwa kurejea kileleni mwa msimamo wa Ligi ya Ufaransa baada ya kulazimishwa sare ya mabao 2-2 na Sochaux muda mfupi uliopita.
Monaco walienguliwa kileleni na PSG, ilianza makeke kwa kutangulia kufunga mabao mawili ya haraka kupitia kwa Ferreira Carrasco aliyefunga katika dakika ya 5 na 10 na kudumu hadi mapumziko.
Hata hivyo wenyeji walicharuka na kurejesha mabao hayo katika kipindi cha pili kupitia Cedric Bakambu dakika ya 57 na Joseph Lopy dakika ya 69 na kufanya matokeo yaishe kwa sare ya 2-2 na kuifanya Monaco kusalia nafasi ya pili ikiwa na pointi 22, mbili nyuma ya PSG.
Michezo mingine inaendelea muda huu katika viwanja kadhaa katika ligi hiyo ya Ufaransa

No comments:

Post a Comment