STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, October 20, 2013

Orlando Pirates yatangulia fainali za Mabingwa Afrika

ORLANDO Pirates ya Afrika Kusini imetangulia Fainali za Ligi ya Mabingwa Afrika baada ya jana kupata sare ya bao 1-1 ikiwa ugenini dhidi ya Esperance ya Tunisia.
Pirates imefuzu fainali hizo kwa faida ya bao la ugenini kwani katika mechi yao ya kwanza iliyochezwa Afrika Kusini timu hizo zilitoka suluhu ya bila kufungana na sare ya jana ina maanisha imefuzu kwa faida ya bao la ugenini linalohesabiwa kama mawili.
Wageni hawakuwa na kazi rahisi kwani walimaliza dakika 45 za kwanza wakiwa 0-0 na kuingia kipindi cha pili kwa kishindo kwa kuwashtua wenyeji baada ya kupata bao la kuongoza lililofungwa katika dakika ya 51 na Rooi Petros Muhamutsa.
Hata hivyo wenyeji walichomoa bao hilo dakika chache baadaye kupuitia kwa Mohammed Iheb Msakni na matokeo kusalia hivyo hadi dakika ya mwisho na kuifanya Pirates kusubiri mshindi wa pambano la leo kati ya wenyeji Al Ahly ya Misri dhidi ya Cotton Sports ya Cameroon, ambazo katika mechi ya awali Wamisiri walilazimisha sare ugenini ya bao 1-1, hivyo kuwa na kazi ya kulazimisha suluhu ili kuungana na Wasauzi.

No comments:

Post a Comment