STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, October 20, 2013

PSG yaua Ufaransa, Ibrahimovic akipiga bao la mwaka

Zlatan Ibrahimovic
MABINGWA watetezi wa Ligi Kuu ya Ufaransa, PSG jana ilitoa kipigo cha mbwa mwizi wakati walipoisulubu Bastia kwa mabao 4-0 na kuiengua Monaco kileleni mwa msimamo wa ligi hiyo kwa muda.
Mabao mawili ya kipindi cha kwanza kutoka kwa mshambuliaji 'mtukutu' kutoka Sweden Zlatan Abrahimovic moja likiwa la aina yake akiunganisha mpira kwa tiktak ya kisigino na kumtungia kipa wa Bastia.
Magoili mengine yalifungwa katika kipindi cha pili na Edinson Cavani na kuifanya PSG ikwee kileleni ikiwa na pointi 24.
Cavani aliifungia PSG bao la nne kwa mkwaju wa penati na kuzima matumaini ya wageni Bastia ambayo imeporomoka hadi nafasi ya 13 katika msimamo wa ligi hiyo.

Hata hivyo huenda mabingwa hao wakaa kwa muda tu katika kiti hicho cha uongozi kabla ya kuwapisha Monaco ambayo muda mchache ujao itashuka dimba la ugenini kupepetana na Sochaux. Monaco ikishinda itarejea kileleni kwa tofauti na mabao ya kufunga na kufungwa.
Katika mechi nyingine za ligi hiyo maarufu kama Ligue 1, juzi Ijumaa Nice iliinyoa Olimpique Marseille kwa bao 1-0, Reims ikilala nyumbani kwa mabao 2-1 mbele ya Toulouse, huku jana Ajaccio ikiwa nyumbani ilikubali kipigo cha bao 1-0 toka kwa Nantes, Evian TG nayo ikilala 2-1 nyumbani dhidi ya Guingamp, nayo Lille ikiicharaza Montpellier bao 1-0 na Rennes na Valenciennes zikitoka sare ya mabao 2-2.
Leo mbali na Monaco kuvaana na Sochaux ugenini, Saint Etienne itaialika Lorient na Olimpicque Lyon itapepetana na wageni wao Bordeaux.

No comments:

Post a Comment