STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, October 20, 2013

Lazio yanyukwa 2-1 na Atalanta, Milan yajitutumua Seria A

 
WAKATI Lazio muda mfupi uliopita imekubali kipigo cha mabao 2-1 toka kwa Atalanta, AC Milan jana iliendelea kujikongoja baada ya kupata ushindi kiduchu wa bao 1-0 ikiwa nyumbani San Siro dhidi ya Udinese.
Bao pekee la Milan lilifungwa na Valter Birsa akimalizia kazi nzuri ya Mbrazil Robinho na kuifanya ifikishe poingti 11 na kuiengua Udinese katika nafasi ya nane na kuishika wenyewe na Udinese ikiporomoka hadi ya tisa.
Mchezo mwingine uliochezwa pia jana, Cagliari iliizima Catania kwa mabao 2-1 kwa mabao ya Ibarbo na Pinilla huku la kufutia machozi la Catania lilifungwa na Bergessio.
Hivi punde tu pambano kati ya Atalanta dhidi ya Lazio limemalizika kwa Lazio ikiwa ugenini kucherzea kichapo cha mabao 2-1.
Cigarini alitangulia kuifungia wenyeji bao katika kipindi cha kwanza bao lilidumu hadi mapumziko kabla ya Brayan Perea kuisawazishia Lazio dakika ya 53, lakini bao la kwenye dakika ya 84 lililofungwa na Dennis liliwapa ushindi wenyeji.
Jioni hii kuna mechi nyingine za ligi hiyo, Juventus ikialikwa na Fiorentina, Inter Milan kupepetana na Torino, huku Genoa kuonyeshana kazi na Chievo.
Mechi nyingine zitakuwa ni kati ya Hellas Verona itakayoialika Parma na Livorno ikiikaribisha Sampodoria.

No comments:

Post a Comment