STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, November 5, 2013

Golden Bush kupongezana Dar kwa kupanda daraja


Kikosi cha Golden Bush Fc walipokuwa wakijiandaa na Ligi daraja la Nne Kinondoni
KLABU ya soka ya Golden Bush inatarajiwa kuwapongezana baada ya vijana wao, kufanikiwa kutwaa ubingwa wa wilaya ya Kinondoni na kupada Ligi Daraja la Tatu.
Golden Bush Fc inayonolewa na nyota wa zamani Madaraka Seleman 'mzee wa Kiminyio', Shija Katina na Wazir Mahadhi 'Mandieta', ikishiriki kwa msimu wake wa kwanza tangu isajiliwe ilifanikiwa kufunika Ligi Daraja la Nne na kupanda daraja.
Kutokana na kitendo hicho, uongozi wa klabu hicho chini ya melzi wao, Onesmo Waziri 'Ticotico' wameamua kuandaa hafla maalum ya chakula cha jioni siku ya Ijumaa kuwapongeza vijana wao.
Kwa mujibu wa taarifa ya uongozi huo, shughuli hiyo itafanyika katika hoteli moja ya jijini Dar es Salaam, ingawa bado hawajaiweka bayana.
"Naomba nitoe taarifa kwamba ule mpango wa kuwa na dinner ya pamoja kama sehemu ya kuwapongeza vijana wetu kwa mafanikio madogo waliyoyapata katika ligi iliyomalizika hivi karibuni, utafanyika siku ya ijumaa tarehe 8 November 2013 hapahapa Dar es Salaam. Bado hujajua sehemu ambayo tutakutana lakini tutaendelea kupeana taarifa juu ya venue ambako event hii itafanyika."
Sehemu ya taarifa hiyo ya uongozi wa klabu hiyo ya Golden Bush maarufu kama Wakali wa soka jijini Dar kwa maveterani inasomeka hivyo. 
 

No comments:

Post a Comment