STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, November 5, 2013

Rage anusuru pambano la Simba vs Ashanti

Ismail Aden Rage
 MWENYEKITI wa klabu ya soka ya Simba, Ismail Aden Rage amefanikiwa kunusuru pambano la timu yake na Ashanti United lililopangwa kufanyika kesho kuchezwa kama kawaida, baada ya awali kutakiwa kulipa kwanza Sh Milioni 25 kama fidia ya uvunjwaji wa viti kwenye uwanja wa Taifa.
Serikali ilitoa adhabu hiyo kwa klabu hiyo kufikiaviti vilivyovunjwa na mashabiki wao wakati wa pambano la Ligi Kuu Tanzania Bara kati yao na Kagera Sugar lililoisha kwa sare ya 1-1.
Kwa mujibu wa taarifa zilizopatikana hivi punde na kuthibitishwa na Afisa Habari wa Simba, Ezekiel Kamwaga ni kwamba Rage alilazimika kuwasiliana na serikali na kuahidi kulipwa kwa fedha hizo mradi waruhusu pambano hilo lichezwe kesho na kufuatiwa na kikao cha pamoja baina ya serikali, Simba na TFF.
Awali TFF ilitumiwa barua toka serikali ikiwataka izuie pambano hilo la Simba na Ashanti United mpaka kwasa Simba walipe fidia hiyo ambayo ilifanywa na mashabiki wao kwa kile kilichoelezwa kukerwa na penati iliyopewa wapinzani wao dakika za lala salama.
"Mechi itachezwa kesho kama kawaida baada ya Mwenyekiti wetu kuweza kuzungumza na serikali kwa ajili ya kukaa chini kujadiliana kuhusu barua hiyo ya kutaka fidia hiyo ilipwe kabla ya kuchezwa kwa mchezo huo." Kamwaga alinukuliwa hivi punde.

No comments:

Post a Comment