STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, November 5, 2013

Mridu Ally aanzisha kundi la Taarab ni Bombastic Modern 'Wana B Kubwa'

Mridu Ally 'TX'
BAADA ya kuyatumikia makundi ya wenzake kwa muda mrefu, hatimaye mtunzi na mcharaza gitaa maarufu wa muziki wa taarab nchini, Mridu Ally 'Tx' ameanzisha kundi lake la miondoko hiyo liitwalo Bombastic Modern Taarab ' Wana B Kubwa'.
Akizungumza na MICHARAZO asubuhi hii, Mridu alisema kundi lake linaundwa na wasanii wasiozidi 10 baadhi wakiwa ni chipukizi na kutamba kama alivyoweza kuwainua chipukizi wengine waliokuja kutamba nchini ndivyo atakavyofanya kwa wasanii hao wapya.
Mrudi alisema kundi hilo linatarajia kuanza rasmi leo kwa kujitambulisha maeneo ya Tabata kabla ya kuendelea katika maonyesho yao ya mwishoni mwa wiki.
"Katika kuhangaika kwangu, nimejianzishi kundi langu binafsi linaliofahamika kwa jina la 'Bombastic Modern Taarab na linaundwa na wasanii kama nane hivyo wengi wao wakiwa ni chipukizi hasa kwa waimbaji, lengo nao kuwainua kama nilivyofanya kwa akina Tizo Mgunda, Salha Abdallah, Sikudhani Ally, Mauji na wengineo," alisema Mridu.
Mridu aliyewahi kulipigia kundi la Mlimani Park 'Sikinde' na kupitia makundi kama Babloom Modern na Dar Modern, alitaja kikosi kizima cha Bombatic kuwa ni yeye (Mridu) kama mpiga solo, gitaa la besi linangurumishwa na Mudi Dirima, na mpapasa kinanda ni Ally Juma 'Za Mkwezi'.
Safu ya uimbaji ina wasanii Mwafatu Mohammed, Nuru Njama, Mwajabu Mtinginya, Fatuma Jafari na Cheka Dadi.
"Tayari tumeshakamilisha baadhi ya nyimbo ambazo trutazitambulisha katika maonyesho yetu ya Jumatano na Ijumaa maeneo ya Tabata kavbla ya Jumamosi na Jumapili kuwepo Mwananyamala na Buguruni," alisema Mridu.
Mridu ndiye mtunzi wa nyimbo zilizowahi kutamba nchini kama 'Acha Shobo' wa Babloom, Pembe la Ng'ombe, Kitu Mapenzi na Malavidavi.

No comments:

Post a Comment