STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, November 29, 2013

Kocha mpya wa Azam kutua nchini kesho

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjYMYRwRJNTdZk47-t9l1I-1h_HV7hn7E52_3lwyskO763mJUnsmohhInBLojgb382ujZiEbi5AusRgouobp1e3wZovcT9ueeANh5NLDPXGmfuvo6AhyphenhyphenVlIPcPY0gAJ3McRRjGzOiFYwKA/s640/Joseph-Marius-Omog-AC-Leopa.jpg
Kocha mpya wa Azam, Joseph Omog anayetua nchini kesho
 KOCHA mpya wa klabu ya Azam, Joseph Marius Omog kutoka nchini Cameroon anatarajiwa kutua kesho asubuhi tayari kumwaga wino wa kuinoa timu hiyo.
Kocha huyo aliyekuwa akiinoa AC Leopards ya Congo Brazaville na kuipa ubingwa wa Kombe la Shirikisho mwaka jana atatua nchini kesho saa 3 asubuhi tayari kumaliza na na mabosi wake wapya.
Iwapo maafikiano yatapatikana, kocha huyo ataanza kuinoa timu hiyo kwa ajili ya duru la pili la ligi kuu na Kombe la Shirikisho itakayoshiriki mwakani kuanzia Jumatatu ambapo kambi ya timu hiyo itaanza rasmi.
Kocha huyo anakuja kuchukua nafasi ya Muingereza Stewart John Hall, aliyetemana na timu hiyo baada ya kupa mafanikio ya kunyakua nafasi ya pili mara mbili katika Ligi Kuu Tanzania Bara na kunyakua vikombe vya Mapinduzi na kucheza Kagame Cup hatua ya fainali.
Kwa mujibu wa akaunti ya klabu ya Azam, mashabiki wanaalikwa kwenda kumpokea kocha huyo kesho atakapowasili kwenye uwanja wa Kimataifa wa ndege wa JK Nyerere.

No comments:

Post a Comment