STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, December 30, 2013

TBF yapata viongozi wapya, Maluwe, Phares chali Dodoma

Michael Maluwe (kushoto) na Magessa waliangushwa jana Dodoma
SHIRIKISHO la Mpira wa Kikapu Tanzania (TBF) limefanikiwa kupata safu mpya ya uongozi baada ya John Bandie kuchaguliwa kuwa Rais Mpya wa shirikisho hilo.
Uchaguzi huo ulifanyika jana mjini Dodoma na kutangazwa na Mjumbe wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT), Jamal Rwambow.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka Dodoma na kuthibitishwa na mmoja wa makocha maarufu wa mchezo huo aliyechaguliwa kuwa Kamishna wa Ufundi na Mashindano Manase Zablon kupitia akaunti yake ya facebook, Rais huyo mpya alipata ushindi huo akimgaragara Phares Magessa.
Magessa alikuwa Makamu wa Rais katika uongozi uliomaliza muda wake ambaye alijikuta akipata kura 19 dhidi ya kura 24 za mpinzani wake aliyeibuka mshindi.
Katika nafasi ya Makamu wa Rais ilienda kwa Hamis Jafar aliyepata kura 39 za Ndiyo huku nne zikimkataa kwani alikuwa mwenyewe katika nafasi hiyo.
Kiongozi maarufu wa zamani wa mchezo huo, Saleh Zonga aliibuka kidedea kwenye nafasi ya Katibu Mkuu, akimshinda aliyekuwa Katibu Mkuu Msaidizi, Michael Maluwe kwa kupata kura 24 dhidi ya 13 za mpinzani wake.
Amina Ahmed alifanikiwa kuchaguliwa kuwa Mhazini wa shirikisho hilo kwa kupigiwa kura za ndito 43, huku Manase Zablon akichaguliwa kuwa Kamishna wa Ufundi na Mashindano kwa kupata kura 37 za ndiyo na mbili kumkataa.
Wengine walishinda katika uchaguzi huo ambao awali ulipangwa kufanyika Desemba 10 mjini Mbeya na kukwama kabla ya kuhamishiwa Dodoma ni Michael Mwita aliyechaguliwa Kamishna wa Mipango kwa kura 39, huku Kamishna wa Watoto na Shule ikienda kwa Patrick Matete, Angela Bondo akichaguliwa Kamishna ya Wanawake na upande wa Walemavu nafasi ilienda kwa Aziz Mtogole.

No comments:

Post a Comment