STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, January 14, 2014

Abiria 48 wanusurika kufa ajali ya basi la Shabiby


ABIRIA wapatao 48 waliokuwa wakisafiri na basi la Shabiby kutoka Arusha kuelekea Dodoma wamenusurika kufa, huku 28 wakijeruhiwa baada ya basi lao kupata ajali.
Basi hilo linadaiwa lilipata ajali wakati likitaka kulipita lori la mafuta wakati basi lingine la Princes Munaa nalo likiwa linalipita basi la Shabiby katika mlima Kisaki na kusababisha basi la Shabiby kuanguka.
Wakieleza kondakta wa basi hilo aina ya Yunton lenye usajili wa namba T 930 BUW ambaye amevunjika miguu yote miwili, Thadei Muhando na mkaguzi wa basi la Shabiby, William Ofyenge wamesema wakati basi lao lilikuwa likilipita lori la mafuta ghafla waliona basi lingine  likiwapita na kuwa magari matatu katika njia moja na hatimaye dereva wao alishindwa kulimudu basi lao na kusababisha kupinduka.
Mganga mfawidhi wa  hospitali ya mkoa wa Singida daktari Banuba Deogratius amethibitisha kupokea majeruhi 28 waliopatiwa matibabu na mgonjwa moja ambaye alikuwa kondakta wa basi amevunjika miguu yote miwili na wanampatia matibabu.
Kwa upande wake dereva wa lori la mafuta aina ya Benz lenye usajili wa namba Raa 496N na tela lake lenye usajili wa namba RL 0255  ambalo lilikuwa likitokea nchi ya Rwanda, Hadimana Benjamini amesema alipitwa na mabasi mawili na moja  likamgonga upande wake na hatimaye kuanguka .
Mkuu wa wilaya ya Singida, Queen Mlozi aliyefika katika ajali hiyo pamoja na kuwatembelea majeruhi amewataka madereva wote kuzingatia sheria za barabarani  ilikuweza kunusuru uhai wa watu na majeruhi. 

No comments:

Post a Comment