STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, January 14, 2014

DR Congo yatakata CHAN yailaza Mauritania 1-0

 DR Congo edge Cameroon to reach CHAN 2014 finals
BAO la mkwaju wa penati lililotupiwa kambani kwenye dakika ya 51 na Emomo Ngoyi imeiwezesha Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo (DRC) kuanza na ushindi kwenye michuano ya CHAN 2014 inayoendela nchini Afrika Kusini katika pambano lililomalizika hivi punde.
Katika pambano hilo lililochezwa kwenye uwanja wa Peter Mokaba, uliopo Polokwane (Pietersburgs) Kongo ikiizamisha Mauritania katika mechi ya kwanza ya kundi D.
Katika pambano hilo timu zote zilionyesha soka la kukamiana na kosakosa za hapa na pale na mpaka mwisho DR Congo walikuwa wababe na kukwea kileleni wakisubiri matokeo ya mechi inayotarajiwa kupigwa muda mfupi ujao kati ya Gabon dhidi ya Burundi kukamilisha mechi za mkondo wa kwanza kwa makundi yote manne yanayoshirikisha jumla ya timu 16.
Kesho mechi za mkondo wa pili utaanza kwa kushuhudia timu za kundi A kutupa karata zao ambapo Nigeria iliyoanza kwa kipigo itapepetana na Msumbiji waliolala kwa mabao 3-1 mbele ya wenyeji Afrika Kusini ambao watakabiliana nna Mali walioitoa nishai Mabingwa wa Afrika (AFCON) Nigeria katika mechi ya fungua dimba siku ya Jumamosi kwa kuilaza mabao 2-1.

No comments:

Post a Comment