STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, January 18, 2014

Arsenal, Man City zaua zikifukuzana England

Edin Dezko
Dzeko akitupia bao la kuongoza

Santi Cazorla (centre) scores the opener for Arsenal against Fulham
Arsenal ilipoiadabisha Fulham kwa mabao 2-0

MABAO mawili ya Santiago Cazorla yaalitosha kuiwezesha Arsenal kuendeleza wimbi la ushindi katika Ligi Kuu ya England na kujichimbia kileleni, huku wapinzani wao wa karibu Manchester City wakiwapumulia nyuma yao baada ya jioni ya leo kutoa kipiogo kingine kizito kwa wapizani wao kwenye ligi hiyo.
Arsenal iliyokuwa nyumbani iliinyoa timu ya Fulham kwa mabao 2-0 kwenye uwanja wake wa Emirates yote yakiwekwa kimiani na Cazorla katika kipindi cha pili na kuifanya timu hiyo ifikishe pointi 51 na kujikitga zaidi kileleni.
Timu inayokamata nafasi ya pili, Man City, iliendelea kugawa dozi kwa wapinzani wake ikipata ushindi wa mechi saba mfululizo baada ya kuinyonyoa Cardiff City kwa mabao 4-2 mabao yaliyofungwa na Edin Dzeko, Jesus Navaz, Yaya Toure na Sergio kun Aguero.
Ushindi huo umeifanya City kufikisha pointi 50, moja nyuma ya vinara Arsenal.
Katika mechi nyingine, Newcastle United ilipata ushindi wa mabao 3-1 ugenini dhidi ya West Ham United, huku Sunderland ikiendelea kuimarika na kutoka mkiani kwa kulazimisha sare ya 2-2 na Southampton, huku Crystal Palace ikikwanyua Stoke City kwa bao 1-0, huku Norwich City ikipata ushindi kama huo mbele ya wageni wao Hull City.
Hivi sasa Liverpool ikiwa nyumbani inapepetana na Aston Villa na matokeo ni sare ya mabao 2-2 baada ya Liverpool kusawazisha hivi punde ikitoka mapumziko ilipokuwa nyuma kwa mabao 2-1.

No comments:

Post a Comment