STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, January 18, 2014

Simba yadonyolewa kimoja na Mtibwa Sugar kirafiki

KIKOSI cha vijana wa Msimbazi, Simba jioni ya leo imejikuta ikipokea kipigo cha pili chini ya Kocha Zdravko Logarusic baada ya kukwanyuliwa na Mtibwa Sugar kwa bao 1-0 katika pambano la kirafiki lililochezwa uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Bao pekee lililoinyamazisha Simba iliyotoka kupokea kipigo cha b aoa 1-0 toka kwa KCC ya Uganda katika fainali ya Kombe la Mapinduzi liliwekwa kimiani na Masoud Ally ‘Chile’ katika dakika ya 64 akimaliza kazi ya Jamal Mnyate.
Kikosi hicho cha Mtibwa Sugar kesho itashuka tena dimbani kwa kuvaana na AShanti United katika pambano jingine la kujiandaa na duru la pili la Ligi Kuu Tanzania Bara itakayoanza wiki ijayo.

No comments:

Post a Comment